• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Tumieni vikao vya Mabaraza Kuzalisha Takwimu sahihi kwa faida ya Taifa: RAS Mwanza

Posted on: December 20th, 2023

Tumieni vikao vya Mabaraza Kuzalisha Takwimu sahihi kwa faida ya Taifa: RAS Mwanza


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Elikana Balandya leo Disemba 20, 2023 amefungua kikao cha tano cha Baraza la sita la wafanyakazi wa ofisi ya Taifa ya Takwimu na kuwataka kutumia vizuri jukwaa hilo kuzalisha Takwimu bora itakayoleta  Maendeleo kwa Taifa.

Akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo kwenye ukumbi wa mikutano Rock City Mall,Balandya amebainisha baraza hilo lina wajibu wa kujenga uelewa wa pamoja wa masuala mbalimbali ya Taasisi na kuhimiza nidhamu kwa upana wake, yote hayo yakifanyika kwa ukamilifu Serikali itaweza kupanga mipango yake ya maendeleo itakayokuwa na tija kwa wananchi.

"Ndugu wajumbe NBS ina jukumu la msingi la kuhakikisha takwimu zinazozalishwa nchini kwa matumizi mbalimbali zinakuwa bora,hivyo baraza hili litasimama kuwa chombo cha kufanya tathmini majukumu mbalimbali yanavyotekelezwa kwa ufanisi,"amefafanua Mtendaji huyo wa Mkoa wakati anazungumza na wajumbe wa baraza hilo wanalokutana kwa siku mbili.

Amewapongeza makamisaa wa Sensa ya watu na makazi 2022,Mhe Anne Makinda kutoka Bara na Mhe.Balozi Mohamed Hamza wa Zanzibar  kwa kusimamia vizuri zoezi la Sensa  iliyofanyika mwaka 2022 ambayo ilikuwa bora.

"Tunamshukuru Rais wetu Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa mafanikio ya Sensa hiyo ambayo ilifanyika katika mazingira ya kisasa ambapo sasa tunawarudishia matokeo yake wananchi kwa kuwaelimisha mipango mbalimbali ya kimaendeleo,"Mhe.Anne Makinda,Kamisaa wa Sensa 2022

Mtakwimu Mkuu wa Serikali Bi.Albina Chuwa amebainisha Sensa ya watu na makazi 2022 ilikuwa ni miongoni mwa Sensa bora ulimwenguni kutokana na kuwa na miundombinu ya kisasa hali iliyoleta ufanisi wa kazi wakati wa zoezi hilo.

Awali kabla ya kwenda kufungua kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Ndg.Balandya Elikana mapema asubuhi aliupokea ugeni Ofisini kwake uliofika kujitambulisha na mazungumzo mafupi ukiongozwa na makamisaa wa Sensa ya watu na makazi 2022, Mhe.Anna Makinda wa Tanzania Bara na Mhe.Balozi Mohamed Hamza kutoka Zanzibar.

Katika mazungumzo hayo Balandya amesema hali ya usalama Mwanza ni shwari na mvua zinazoendelea kuonyesha hazijaleta madhara makubwa gkulinganisha na mikoa mingine zaidi ya mafuriko ya muda mfupi kwa waliojenga kwenye njia za asili za maji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.