• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWANZA UTAKUA WA AMANI : MTANDA

Posted on: November 6th, 2024

UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWANZA UTAKUA WA AMANI : MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa viongozi wa dini mkoani humo kuendelea kuhamasisha wananchi kujiandaa kushiriki kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utakua huru kwani utazingatia sheria na kanuni za uchaguzi.

Ametoa wito huo leo Novemba 06, 2024 wakati akihutubia kongamano la viongozi wa dini kutoka kamati ya amani ya Mkoa wa Mwanza lililofanyika mahususi kuhamasisha upigaji kura kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa wa Novemva 27, 2024.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Mwanza umejipanga kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za mitaa unakua wa haki, uhuru na amani kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu za uchaguzi na kwamba wananchi wanapaswa kujiandaa kushiriki bila hofu yoyote.

"Mkoa wa Mwanza tulilenga kuandikisha watu milioni 1.9 lakini tumeandikisha watu milioni 2.86 sawa na asilimia 106 na tumeshika mafasi ya 3 kwa mikoa , nawashukuru sana viongozi wa dini kwa hamasa yenu na nitaendelea kushirikiana nanyi kila siku."

Vilevile, amewataka wananchi kujiepusha na mizengwe ya uchaguzi na kutowekeana mapingamizi yasiyo na sababu baina ya chama kimoja na kingine na kwamba ni lazima wasimamizi wa uchaguzi huo wamtangaze mshindi mara moja bila kusubiri jambo lolote.

Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya amani amesema uchaguzi upo kwenye vitabu vya dini hivyo viongozi wa dini wanapaswa kuhakikisha wanahamasisha wananchi kushiriki tena kwa amani.

Mwenyekiti Mwenza Kamati ya Amani ya Viongozi wa dini Mkoa wa Mwanza  Askofu Charles Sekelwa amesema demokrasia siyo haki tu ya kupiga kura bali pia nafasi ya wananchi baada ya kusikiliza sera kuamua ni nani wamchague kwani watakua wameshajua nini atawapatia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.