• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

UFUGAJI WA KISASA WA SAMAKI UTAONGEZA TIJA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI :NAIBU WAZIRI

Posted on: August 13th, 2024

UFUGAJI WA KISASA WA SAMAKI UTAONGEZA TIJA KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI :NAIBU WAZIRI


Mkutano wa tatu wa ukuzaji viumbe maji Afrika Mashariki umefunguliwa rasmi leo Agosti 13, 2024 Jijini Mwanza na rai imetolewa ya kutolewa kwa elimu ya ufungaji wa kisasa wa samaki kwa njia ya vizimba.

Akifungua mkutano huo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe.Alexander Mnyeti amesema uvuaji holela umepitwa na wakati na umesababisha samaki wengi kupotea wakiwemo Ningu na Gobogobo.

Mnyeti amebainisha kuwa licha ya ziwa hilo sehemu kubwa kuwa Tanzania lakini bado hatujalitumia vizuri kulinganisha na wenzetu wa nchi jirani kama Uganda.

"Huku kwetu tuna jumla ya vizimba 168 hivi kwenye ziwa Victoria na Tanganyika lakini Uganda wao wana vizimba zaidi ya 2000, hapa tunaona bado tunahitaji mkazo wa kuelimishana", Mhe. Mnyeti.

Amesema, Serikali imeweka mazingira mazuri katika sekta ya uvuvi kwa kutoa fursa za mikopo bila riba kutoka benki ya TADB lengo likiwa ni kufanya shughuli hiyo kwa tija.

Amezitaka pia taasisi zinazojihusisha na maendeleo ya ziwa Victoria kuzidi kubuni mikakati ya kuwalinda viumbe maji kwa kulipumzisha ziwa hilo na shughuli za uvuvi.

Akitoa salamu fupi za Mkoa wa Mwanza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masalla ameishukuru Serikali ya Rais Samia kwa kuzidi kuiboresha sekta ya uvuvi na ajira kwa ujumla.

"Zaidi ya Tshs bilioni tano zimeletwa Mwanza, boti 26 za kisasa pamoja na vizimba 16, hii imechangia kuongeza tija katika sekta hiyo", ameeleza Mhe.Masalla.

Jumla ya Mataifa 18 yanashiriki mkutano huo zikiwemo Uganda, Kenya, Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na Nigeria.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.