• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Uhusiano baina ya Tanzania kichocheo cha kuinua uchumi-Balozi Chen

Posted on: September 9th, 2023

Uhusiano baina ya Tanzania kichocheo cha kuinua uchumi-Balozi Chen


Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania Mhe.Chen Mingjian amesema Tanzania na China zitaendelea kufaidika na uhusiano mzuri ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere na Mao Tsetung katika kuinua uchumi wa nchi hizo kupitia nyanja mbalimbali.

Balozi Chen amezungumza hayo leo Mkoani Mwanza akiwa na timu ya wabunge kumi kutoka Bunge la Tanzania ambao ni marafiki na Bunge la China mara baada ya kuhitimisha ziara yake fupi ya kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Kampuni ya kutoka nchini kwake ya CCECC inayojenga Daraja la JP Magufuli na mradi wa Reli ya kisasa SGR kipande cha tano kutoka Isaka kuja Mwanza.

Balozi Chen amesema Makampuni 17 kutoka China yapo nchini kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni matokeo chanya ya mahusiano ya nchi mbili zenye mahusiano adhimu.

Ameongeza kuwa amefurahishwa kuona wataalamu kutoka Tanzania wanafanya kazi bega kwa bega kwenye mradi wa Daraja la JP Magufuli kwa lengo la kupata ujuzi zaidi ili kuja kuwa tegemeo katika miradi ijayo.

"Nchi yangu inanufaika sana kutokana na mahusiano mazuri tuliyonayo,tupo katika kujiimarisha na lugha ya kiswahili ili kufundisha kwenye vyuo vikuu vyetu na sehemu nyingine, watu kutoka China wapo hapa Tanzania kujipatia taaluma hiyo,"amesisitiza Balozi Chen.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa urafiki wa Wabunge baina ya Tanzania na China Mhe.Dkt.Charles Kimei,Mbunge wa Masasi mjini Mhe.Geofrey Mwambe amesema mradi wa Daraja la JP Magufuli na Reli ya kisasa utakuwa kitega uchumi cha uhakika kutokana na Mwanza kuwa na jirani na nchi za  maziwa makuu.

"Sina shaka yoyote na uwekezaji unaofanywa na China kwenye nchi yetu siku za nyuma nimekuwa Mtendaji Mkuu wa kituo cha uwekezaji nafahamu vizuri Tanzania tunavyonufaika,"Mhe.Mwambe.

Mradi wa Daraja la JP Magufuli uliyogharimu bilioni 716 unatarajia kukamilika Disemba mwakani wakati Reli ya kisasa SGR kipande cha kutoka Isaka hadi Mwanza wenye gharama ya zaidi ya Trilioni 3 utakamilika Mei mwakani.

Akiwa kwenye mradi wa SGR Wilayani Kishapu,Balozi Chen ametembelea kiwanda cha  kufyatua mataluma ya Reli na kuzungumza na wafanyakazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.