• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Usagara yapata Usafiri wa moja kwa moja

Posted on: May 3rd, 2018


Wananchi wa Usagara na maeneo jirani wilayani Misungwi mkoani Mwanza wanatarajia kupata neema ya usafiri wa moja kwa moja utakaowafikisha katika hospitali ya mkoa Sekou Toure na katikati ya jiji.

Hayo yalisemwa jana na Ofisa Leseni na Mkaguzi wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) mkoa wa Mwanza ,Daniel Chilongani kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali ,dini na wanasiasa kilichofanyika mkoani hapa alisema wapo katika hatua za awali za kuanzisha safari (roote) ya daladala ambazo zitakuwa za Usagara – Mzunguko zitakazokuwa zinapita katikati ya jiji na kuishia hospitali ya mkoa.

Chilongani alisema, wameamua kuja na mpango wa kuanzisha safari ( roote) hiyo ili kuwasaidia na kutatua changamoto ya usafiri kwa wananchi wa Usagara, kwani wakitaka kupata huduma katika hospitali ya Mkoa wanatumia gharama kubwa kwa ajili ya nauli na wanapata usumbufu wa kutumia gari zaidi ya moja kufika eneo husika.

Alisema, Sumatra katika kuhakikisha inaondoa hadha ya usafiri kwa wananchi wanategemea kuanzisha safari (roote) nyingine ambayo itatoka Kigongo Ferry kupitia katikati ya jiji hadi hospitali ya mkoa ambapo magari yatakuwa ni Kigongo Ferry – Mzunguko ambayo yatahusisha magari makubwa ( mabasi makubwa) yenye uwezo wa kubeba abiria kuanzia 25.

Pia alisema safari (roote) hiyo itasaidia kupunguza msongamano wa daladala katikati ya mji pamoja na kuwapa fursa wananchi ya kupata usafiri na kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi, ili waweze kuendelea katika shughuli za kimaendeleo na kupata huduma muhimu zinazopatikana makao makuu ya mkoa.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Madereva Kanda ya ziwa, Hassan Dede alisema sumatra wanapoanzisha safari (roote) mpya washirikiane kwa pamoja katika kuhakikisha wanaelimisha madereva na kubandika stika zinazoonyesha mwanzo hadi mwisho wa safari.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.