• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Uunganishwaji wa Meli mpya ya MV.Mwanza Hapa Kazi Tu waanza

Posted on: September 16th, 2020


Ujenzi rasmi wa meli kubwa kabisa katika ziwa Victoria waanza rasmi Baada ya kukamilika kwa uwekaji wa mkuku ( Keel Laying ) wa meli mpya ya "Mv.Mwanza hapa kazi tu "inayojengwa katika chelezo.

Akizungumza katika hafla hiyo leo  Ofisa mtendaji mkuu wa kampuni ya huduma za meli ( MSCL) Eric Hamissi anaeleza kuwa hiyo ndio hatua ya kuanza kwa ujenzi na uunganishaji wa msingi wa meli ili kupata msingi wote wa meli ,ambapo kwenye msingi huo utakuwa na kwenye vipande na una  kina cha mita 3.75 ambacho ufikiwa wakati meli imebeba mzigo wote.

" Kukamilika kwa msingi huu wa meli kutawezesha ujenzi wa meli kwenda kwa kasi kuliko kasi ya awali ,kutokana nausanifu bora wa meli hii kampuni yetu inampango wa kuweka kumbukumbu za mradi mzima wa ujenzi wake katika maktaba zake kwa ajili ya vizazi vijavyo " anaeleza Hamissi

Ameongeza kuwa kampuni inayofanya kazi ya ujenzi wa meli hiyo inaitwa GAS Entec, na kampuni ya KANGNAM Corporation zote kutoka Korea ya Kusini zikishirikiana na SUMA JKT ya Tanzania kwa gharama ya Dola za kimarekani 39,000,000 sawa na shilling Billion  89.764 hadi sasa mradi umefikia kiasi cha asilimia 68 kwa ujumla wake na serikali imeshamlipa mkandarasi jumla ya shilingi za kitanzania billion 59.896 sawa na asilimia 68 ya gharama zote za mradi.

Naye Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya Uchukuzi) Mhandisi Dk Leonard Chamiriho anasema hiyo ni hatua ya kwanza muhimu kwa maisha ya meli ,pia mpaka Sasa miradi mitatu imekamilika ambayo ni mradi wa Mv.Victoria ambayo kwa sasa inafanya safari zake kutoka Mwanza kwenda Bukoba, ukarabati wa mkubwa wa Mv.Butiama na mradi wa chelezo.

" Mji wa Mwanza umenufaika na ujenzi wa meli hii kwani imetoa ajira kwa wingi lakini hapa tulipo Septemba 3 mwaka 2018 ilitiwa saini mikataba ya miradi minne ambapo miradi mitatu imekamilika " ameeleza Chamiriho.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella amewahakikishia usalama katika mkoa wake ili kazi zifanyike kwa utulivu na ueledi unaotakiwa ,pia ujenzi huo wa miundombinu ya kimkakati ya kiuchumi ni hatua moja wapo nyeti ya kufikia lengo.

" Juzi Rais Magufuli alipofika Mwanza kufanya Kampeni aliwaeleza wananchi nia yake ya dhati na ya serikali kuifanya Mwanza kuwa kitovu cha kiuchumi kwenye Kanda za maziwa makuu na lengo hilo litatimia" anaeleza Mongella.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.