• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Viongozi wa Umma waaswa kujiepusha na migongano ya maslahi

Posted on: May 5th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima ameziagiza halmashauri zote zilizopo mkoani humo kutoa mafunzo kwa Viongozi wa umma ili kuwakumbusha kutenda kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, maadili na uadilifu wa utumishi wa umma.

Mhe. Malima amesema kumekuwa na mmomonyoka mkubwa wa ukiukwaji maadili kwa baadhi ya  watumishi wa umma   wanapotekeleza majukumu yao ikiwemo miradi ya maendeleo hali inayosababisha itekelezwe chini ya kiwango ikiwa haina thamani halisi ya fedha.

 Mhe. Malima ameyasema hayo leo Mei 5, 2023 wakati akifungua mafunzo ya maadili kwa viongozi wa umma wa Mkoa wa Mwanza yaliyolenga kuwakumbusha viongozi na wakuuu wa taasisi za umma mkoani humo kuzingatia kanuni, sheria na taratibu wakati wa kutekeleza majukumu yao, kujiepusha na masuala yote yanayoweza kuwaingiza kwenye mgongano wa maslahi na kuzingatia suala la uwajibikaji wa pamoja.

“Maadili ni nguzo muhimu sana katika kufanikisha mipango ya maendeleo, viongozi wa umma zingatieni hilo hasa zile Taasisi zinazotekeleza miradi  mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi  kwa mfano MWAUWASA, TARURA, RUWASA, TANESCO na REA mnapokosa uadilifu mkakoroga mradi anayetukanwa na wananchi ni Mhe. Rais na Chama cha Mapinduzi wakati lengo la Serikali ni kuinua maisha ya wananchi kiuchumi ndani ya mkoa wa Mwanza sitawavumilia”amesema Mhe. Malima.

Naye, Katibu Msaidizi wa Sekretarieti ya  Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa, Godson Kweka, amesema mafunzo hayo yana mada tatu ambazo ni Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ambapo wanakumbushana misingi ya Maadili ya Umma kama ilivyoainishwa kwenye Sheria hiyo, mgongano wa maslahi na Uwajibikaji wa pamoja katika kuwaletea wananchi maendeleo.

“Tunawakumbusha Viongozi wa Umma Mkoa wa Mwanza kuishi na kuheshimu viapo vyao vya ahadi ya uadilifu walivyoapa kwa nyakati tofauti walipopewa dhamana ya nafasi walizonazo kwa sasa kipaumbele kikubwa cha  sekretarieti ya maadili ya umma pamoja na mambo mengine ni kuhimiza suala zima la uwajibikaji wa pamoja kwa viongozi, watumishi na wananchi katika ushirikishwaji ili kuwaletea wananchi maendeleo,”amsesema na kuongeza.

“Sisi sote ni mashahidi, hatuna shaka na tunakila sababu ya kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi anavyotafuta fedha za kutekeleza miradi mbalimbali  katika halmashauri zetu  kwa ajili ya  kuwaletea wananchi maendeleo  miradi hiyo inahitaji kuwa na viongozi waadilifu kwenye usimamizi wa fedha na usimamizi wa rasilimali zingine ambazo zipo kwenye maeneo yao ya kazi.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Balandya Elikana, amewataka watumishi wa umma  kufanya kazi kwa uadilifu na kuwa wazalendo ili kukidhi matarajio ya wananchi kwa serikali yao katika kuwaletea maendeleo.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.