• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TEHAMA kutatua changamoto Mkoa wa Mwanza

Posted on: January 23rd, 2018


Wabunifu wa TEHAMA kutatua changamoto mbalimbali Mkoa wa Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amefungua kikao cha wabunifu wa Tehama katika kutatua baadhi ya  changamoto zinazoukabili Mkoa wa Mwanza kilichofanyika katika Ukumbi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ikiwa ni juhudi zake za kukuza ubunifu na kukabiliana na changamoto mbalimbali nchini, ambapo kikao hicho kimefadhiliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi(COSTECH) kwa kushirikiana na (Atamizi) DTBi, ikiwa ni mwendelezo wa mpango wa kuibua vipaji vya ubunifu katika Tehama kwa kutumia vijana wabunifu kutoka Mkoa wa  Mwanza.

Kikao hicho kimewapa fursa vijana waliochaguliwa kutatua changamoto mbalimbali za Mkoa wa Mwanza, kuwasilisha mada zao ambazo zina lengo la kutoa suluhisho la changamoto mbalimbali kwa kutumia matumizi ya Tehama, ambapo kimehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma, sekta binfsi ( wavuzi, wakulima, wafanyabiashara) CTI, TCCIA, vyombo vya ulinzi na usalama, wataalamu kutotka ngazi ya Mkoa na Halmashauri za Ilemela na Nyamagama.

Suala la usalama ziwani lilichangiwa na wadau wengi kwani asilimia kubwa ya aeneo yanayozunguka ziwa Victoria ni wavuvi hivyo basi, mada iliwasilishwa kwa wadau na kugundua kuwa kuna changamoto mbalimbali zinazowakabili wavuvi na tatizo kubwa ni uvuvi haramu ndani ya ziwa Victoria unahatarisha mazalia ya samaki, pia uhalifu huu huandamana na suala la usalama wa vyombo vya usafiri ndani ya ziwa kwani mara kwa mara wavuvi wamekuwa wanaibiwa injini za vyombo vyao na kunyang’anywa samaki.

 Baada ya kubaini changamoto hizo wataalamu wamekuja na mfumo ambao ni suluhisho la changamoto hizo kwa wavuvi na kwa sasa uko katika hatua za majiribio mara tu utakapokamilika utatumika kutatua shida za wavuvi za kiusalama na hivyo kupunguza na kudhibiti uvuvi haramu na uharamia ziwani.

Mfumo wa kukabiriana na changamoto za foleni za magari barabarani umeshatengenezwa, uko katika hatua za awali za majaribio, inatarajiwa kuwa jeshi la pilisi litatumia mfumo huu utakaobaini magari yasiyofuata sheria barabarani, kubaini ajari barabarani,kwa kuwa kutokana ka kukua kwa Jiji la Mwanza,msongamano wa watu na magari umeongezeka hivyo mfumo huu utatatua tatizo hilo, kwani  watumiaji wataweza kupata taarifa ya barabara zenye msongamono mkubwa na hivyo kutafuta njia mbadala, hii itapatikana kwa kutumia simu za mikononi kwa wale watakaokuwa wamejisajiri kwa mfumo huu.

 Mkoa wa  Mwanza ni miongoni mwa mikoa yenye fursa nyingi katika maeneo ya ufugaji samaki, kuku na kilimo cha mboga mboga na matunda, ubora wa mazao kwa wazalishaji bado uko chini jambo linalowafanya wazalishaji kutokupata masoko ya uhakika yanayowawezesha kukuza kipato chao, hivyo mfumo umeundwa utakaobaini changamto zilizopo katika jiji la Mwanza, na  utasaidia wajasiriamali katika maeneo mbali mbali kupata elimu na majibu ya changamoto zinawakabili hasa katika ufugaji wa samaki, kilimo cha mboga mboga, matunda na ufugaji wa kuku wa kisasa na kienyenyeji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.