• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wadau wa kilimo,Mifugo,Uvuvi wakutana kutatua changamoto, kuangalia fursa

Posted on: September 19th, 2019


Wadau hao wamekutana leo katika kikao kilichofanyika jijini Mwanza na kuhudhuriwa na taasisi za kifedha, taasisi za serikali, mashirika yasiyo ya serikali, Makampuni ya huduma za pembejeo na zana za kilimo pamoja na Makampuni ya usindikaji, na kuongozwa na mwenyekiti wa kikao hicho, Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John V. K Mongella huku dhumuni likiwa ni kuwakutanisha wadau hao ili kuweza kubadilishana ujuzi wa kazi wanazozifanya.

 Akizungumza katika kikao hicho Mhe.  Mongella amewaeleza wadau hao  kujikita katika kilimo cha mazao ikiwemo kilimo cha alizeti,  pamoja na kilimo cha pamba na kujiuliza  swali, nimefanya nini katika kukuza sekta za kilimo, uvuvi na mifugo.

" Nipende kuwashauri wadau kujikita hasa katika kilimo cha mazao, ikiwemo kilimo cha alizeti mamoja na kilimo cha pamba".

Aidha Mhe.  Mongella amebainisha kuwa sekta ya kilimo imekuwa na mipango ya kuondoa umaskini, kuongeza usalama wa chakula na kuongeza pato.

"Sekta ya kilimo ina mpango wa kuondoa umasikini, kuongeza usalama wa chakula,  ubora wa lishe na kuongeza pato kuanzia kwa mtu mmoja mmoja, kwenye kaya, jamii mpaka taifa,"alisema Mongella.

 Naye Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Christopher Kadio amebainisha kuwa kikao hicho kitatoa nafasi kwa wadau mbalimbali kupata fursa ya kufahamu changamoto zinazoikabili sekta ya kilimo, uvuvi na mifugo katika mkoa wa Mwanza.

"Wadau mbalimbali  watapata fursa ya kufahamu changamoto zinazoikabili sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi katika mkoa wetu wa Mwanza,"alisema Kadio.

Aidha Meneja wa Benki ya NMB tawi la Pamba Road, Dotto Alex Makota, ameeleza kuwa wanashiriki kikamilifu katika huduma za kifedha kwenye kilimo kwa kutoa mkopo wa pesa katika sekta ya kilimo ili kuhakikisha wakulima wananufaika.

"Sisi kama NMB tunashiriki kikamilifu katika huduma za kifedha kwenye kilimo, na asilimia 35 ya pesa ya NMB inakwenda katika kilimo kwa kutoa mikopo kwa  wakulima," alisema  Makota.

Aidha Mwenyekiti wa wafugaji Wilaya ya Sengerema  Clement Mathayo amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikumba sekta hiyo ikiwemo kukosekana kwa maeneo ya kutosha kwa ajili ya malisho,  maji na  kukosekana kwa soko la uhakika.

"Wadau wa ufugaji tunakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kukosa soko la uhakika,  maeneo kwa ajili ya malisho na maji, tunaomba Serikali itutazame kwa upana,"lisema Mathayo.

Pamoja na hayo Mhe. Mongella amewashauri viongozi kuweza kutoa nafasi kwa wananchi wao ili kuweza  kuzungumza na kueleza changamoto zinazowakabili katika sekta mbali mbali wakati wa vikao vyao na wananchi, pia amewataka wadau  kuwa mfano kwa kuweza kutekeleza majukumu yao kwa vitendo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.