• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wadau wa Sekta ya Maziwa punguzeni bei ili mpango wa kunywa Maziwa shuleni ufanukiwe : Naibu Waziri Mnyeti

Posted on: September 27th, 2023

Wadau wa Sekta ya Maziwa punguzeni bei ili mpango wa kunywa Maziwa shuleni ufanukiwe : Naibu Waziri Mnyeti


Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewaomba wadau wa tasnia ya maziwa nchini kupunguza bei ya maziwa ya Shs 1800 kwa nusu lita ili mpango wa kunywa maziwa watoto wote shuleni ufike malengo.

Kauli hiyo imetolewa leo kwenye viwanja vya Furahisha Mkoani Mwanza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya unywaji maziwa shuleni Duniani ambapo Kitaifa imefanyika Mkoani humo.

Mhe. Mnyeti amesema Serikali imefuta tozo zote zinazohusu maziwa hivyo  mamlaka husika ziangalie bei muafaka eneo la vifungashio ili wadau wa tasnia hiyo wasiingie gharama kubwa.

"Bado Mkoa kama wa Mwanza unakabiliwa na hali ya udumavu wa watoto hii imechangiwa na ukosefu wa lishe bora, hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha unywaji wa maziwa uwe sehemu ya mlo wa mtoto shuleni." amesisitiza Mhe.Mnyeti.

Amesema itakuwa ni kazi bure kuendelea kuhimiza unywaji wa maziwa kila Ifikapo kilele cha maadhimisho hayo wakati uwezo wa kumudu hali hiyo haupo kutoka kwa wazazi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi ameishukuru Wizara kwa kuona umuhimu wa maadhimisho hayo kufanyika Mkoani humo kutokana na miradi mingi ya kuboresha mifugo inatekelezwa kuanzia Shamba la Taifa la Mifugo Mabuki na kwenye baadhi ya wilaya.

"Mhe. mgeni rasmi Serikali ya awamu ya sita imeleta mitamba 500 Mkoani Mwanza kwa ajili ya kuleta tija ya maziwa na nyama kwa wafugaji, pia wapo vijana wanaopatiwa mafunzo maalum ya ufugaji wa kisasa huko Mabuki," Mhe.Makilagi.

"Bado tuna changamoto ya unywaji wa maziwa nchini ambapo hadi sasa mtu mmoja anakunywa lita 62 kwa mwaka wakati kwa mujibu wa mwongozo wa kimataifa mtu mmoja anatakiwa kunywa lita 200 kwa mwaka, hivyo inahitajika kazi ya ziada kuhamasisha jamii umuhimu wa kunywa maziwa," Dkt.George Msalia,Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini TDB.

Kuelekea kilele hicho Bodi ya Maziwa ilifanya zoezi la ugawaji wa maziwa shuleni na utoaji wa elimu kwa baadhi ya shule Mkoani Mwanza pamoja na kufanya kongamano lililowahusisha wadau wa tasnia ya maziwa na walimu.

Kila  Jumatano ya mwisho wa Septemba Tanzania inajumuika na Mataifa mengine ulimwenguni kuadhimisha siku ya unywaji maziwa shuleni ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema "Mpe mtoto maziwa kwa maendeleo bora Shuleni"

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.