• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

"Wafanyabiashara waliopisha ujenzi wa Stendi kuu ya Nyegezi wapewe kipaumbele" Mhe Majaliwa

Posted on: October 18th, 2022


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ameutaka uongozi  wa Halmashauri ya jiji la Mwanza kuhakikisha wafanyabiashara wote waliokuwa wanafanya biashara Stendi Kuu ya zamani ya mabasi yaendayo mikoani ilipojengwa mpya katika Kata ya Nyegezi wapewe  kipaumbele kupata maeneo ya kufanyia biashara.

Mhe.Majaliwa ametoa agizo hilo  Oktoba 17,2022 wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa stendi hiyo  inayojengwa  kwa fedha za serikali Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza kwa gharama ya Sh bilioni 15,885,589,063 na mkandarasi Mohammedi Builders Ltd.

"Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya kimkakati lengo ni kuwanufaisha wananchi wake na mmeniambia kwamba mmejenga stendi hii nzuri kabisa ya  kifahari  lakini kuna eneo limebaki hivyo endapo maeneo yaliyopo ndani ya stendi hii yatakuwa machache kuwatosha wafanyabiashara wote  waliokuwa wakifanya biashara zao hapa awali wajengeeni kwenye eneo hilo.

" Maana Rais Samia Suluhu Hassan ameleta Shilingi bilioni tisa katika jiji la Mwanza kwa ajili ya kujenga masoko  nia na dhimira yake ni kuwaandalia na kuwajengea  machinga maeneo yao ili wafanye biashara zao katika mazingira  bora, amesema na  nyie wafanyabiashara mliokuwa mnafanya biashara kwenye stendi hii zamani kabla ya ujenzi wa hii mpya haujaanza kama kwa sasa hautafanya tena biashara  toa taarifa kwenye uongozi wa jiji ili wengine wanaohitaji wagawiwe maeneo usikae kimya,"ameagiza Mhe. Majaliwa.

Aidha, amewataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza wajipange kwa ajili ya

kunufaika na miradi mikubwa ya kimkakati inayojengwa mkoani humo ikiwemo ujenzi wa Reli ya kisasa(SGR), daraja la kigongo busisi maarufu kama Daraja la J.P Magufuli, stendi hiyo ya Nyegezi na iliyojengwa Wilaya ya Ilemela ambapo amewahakikishia wananchi kwamba hakuna mradi wowote wa kimkakati unaotekelezwa ndani ya mkoa huo  utakaokwama  maana fedha zipo na tayari serikali imeishazitenga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Yahya Sekiete amesema hadi sasa  mradi huo umetekelezwa kwa asilimia 98 ingawa ulikumbwa  na changamoto mbalimbali zikiwemo upatikanaji wa vifaa vya ujenzi kama saruji, nondo kutokana na kupanda kwa bei, bati za geji 26 zilizokuwa hazipatikani nchini pamoja na baadhi ya vifaa vinavyoagizwa nje ya nchi kuchelewa kufika bandarini.


" Mradi huu ulianza kutekelezwa Februari 5, 2019 ukikamilika utasaidia kuongeza mapato ya halmashauri ya jiji la Mwanza hivyo kupunguza utegemezi kutoka serikali kuu pia utalifanya jiji la Mwanza kuwa la kisasa zaidi, utasaidia kukua kwa biashara nyingine kutoka mikoa mbaimbali  na nchi jirani.

Ametaja maeneo yatakayokuwepo baada ya mradi huo kukamilika kuwa ni pamoja na  eneo la maegesho ya mabasi 120, madogo 80 kwa wakati mmoja, maduka makubwa 14, madogo 60, sehemu tatu za abiria  wapatao 7400 kusubiria mabasi, vyoo saba vyenye matundu 63 jengo la abiria, benki, vibanda 38 vya kukatia tiketi na vibanda vya mama lishe na eneo maalum kwa ajili ya wanawake wanaonyonesha.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.