• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAGONJWA KIPINDUPINDU MWANZA WAPUNGUA-RC MAKALLA

Posted on: January 24th, 2024

WAGONJWA KIPINDUPINDU MWANZA WAPUNGUA-RC MAKALLA


*Asema kuna mpya 1 na waliolazwa 7 tu Mkoani Mwanza*


*Awataka TARURA kuondoa maji yaliyotuama kwenye mitaro*


*Asema kwenye mikusanyiko tuzingatie usafi na kanuni za afya kutokomeza Kipindupindu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema Maambukizi ya ugonjwa wa Kipindupindu Mkoani yamepungua sana kwani kuna mgonjwa mpya mmoja tu ambapo saba pekee wakiwa hospitali wamelazwa kwenye maeneo mbalimbali na akawataka wadau kuendelea na mikakati ya kuthibiti kusambaa.

Mhe. Makalla amebainisha hayo mapema leo Januari 24, 2024 wakati wa mkutano wake na Mganga Mkuu wa Serikali,Prof.Tumaini Nagu uliofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huku ukiwakutanisha viongozi wa Taasisi mbalimbali za Serikali za Mkoa huo.


Makalla amesema ni lazima kuendelea na mikakati ya kuthibiti kusambaa kwa maradhi hayo huku akitaja afua ya kuzibua mitaro ili maji ya mvua yasituame na kufikia hatua ya kusambaa kwenye makazi ya watu.

Akibainisha namna tatizo hilo lilivyo dhahiri Makalla amesema tangu kuibuka kwa ugonjwa huo juhudi mbalimbali zimefanywa kuudhibiti na akatumia wasaa huo kukemea tabia ya kuishi kwa mazoea hususani kwenye tabia za ulaji wa vyakula bila kuosha hasa Matunda.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu amewataka wadau wa afya na viongozi wengine kuzingatia sheria ndogondogo za Serikali za mitaa ili kuhakikisha afya ya jamii inazingatiwa hususani kwenye makundi kama ya mialo ya uvuvi.

"Ukiugua kipindupindu maana yake umekula mavi mabichi, aidha kwa uchafu kupitia kula kinyesi chenyewe au kupitia vitu mbalimbali tunavyoweka mdomoni kwa mikono isiyo safi, hivyo ni lazima watu wanawe mikono kwa maji safi na salama tena kwa Sabuni wakati wote" Prof. Nagu.

Halikadhalika, Mganga Mkuu ametoa wito kwa jamii kula vyakula vya moto, kuosha matunda na kunawa mikono kwa naji safi na salama yanayotiririka na kwa sabuni ili kukomesha kabisa janga hilo ndani ya Mkoa na ukanda huo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.