• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wahujumu Pembejeo za kilimo Wakamatwa Mwanza

Posted on: May 8th, 2020

Mhasibu wa AMCOS ya MHEDI iliyopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga na wafanyabiashara 13 na madalili 3  washikiliwa na TAKUKURU Mwanza kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa kinyume na sheria.


Akitoa taarifa hiyo Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mwanza Emmanuel Stenga alisema Mhasibu Paulo Nkuba alikuwa akisafirisha na kuuza dawa za kilimo zilizonunuliwa na serikali na kupelekewa Bodi ya pamba kwa lengo la kuwapatia wakulima wa pamba kupitia vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kwa madalali na wafanyabiashara wa maduka ya pembejeo za kilimo maeneo ya Lumumba Jijini hapa .

Alisema TAKUKURU ilifanya upekuzi kwenye madauka ya bembejeo za kilimo baada ya kupata taarifa kutoka bodi ya pamba na kubaini kuwa dawa hizo zenye thamani ya shillingi 12,609,000 zimeuzwa kwa wafanyabiashara hao kinyume na utaratibu .

"Baada ya kubaini changamoto hiyo tumefanya ufatiliaji na kutambua kwa nini pembejeo za kilimo haziwafikii wakulima kwa wakati kumbe kuna baadhi ya viongozi wa AMCOS wasio waadilifu wamekuwa wakiyauza madawa hayo kwa njia ya rushwa pia tumefatilia na madeni ya wakulima wa AMCOS na tumeweza kuokoa fedha nyingi ambazo zimehujumiwa na baadhi ya viongozi mbalimbali mkoani hapa"alisema Stenga.

Aliongeza kuwa baadhi ya viongozi hao wamekuwa wajizifanyia hujuma fedha za serikali kwa kuandaa vocha za usambazaji wa pembejeo hizo na kudai fedha nyingi serikali sambamba na kuwakata fedha wakulima na kutoziwasilisha serikalini pamoja kuwauzia wafanyabiashara badala ya wakulima.

Alisema watuhumiwa wote wamekwenda kinyume na kifungu 15 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11/2007 pamoja na kupatikana kwa mali njia isiyo halali kinyume na kifungu cha 311 cha sheria ya kanuni ya adhabu na marekebisho yake ya mwaka 2002 hivyo uchunguzi wa tuhuma hizo bado unaendelea kwa kuwabaini wote wanaohusika na ubadhirifu huu pindi uchunguzi utakapokamilika wahusika wote watafikishwa kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma ziazowakabili.

Aliongeza kuwa zoezi hilo ni endelevu na hawatovumilia kuona upotevu wa fedha za serikali pia waliwataka wafanyabiashara wote kuacha tabia hiyo vinginevyo hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kuhusika na ubadirifu wa pembejeo za kilimo ,aidha wakulima watoe ushirikiano kwa TAKUKURU pindi wanapoona mambo hayaendi kwa utaratibu uliokusudiwa.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa huo Mhe.John Mongella baada ya kupokea taarifa hiyo alisema tumeona pembejeo zilizokamatwa ambazo ni ruzuku ya serikali zinazotakiwa kwenda kwa wakulima moja kwa moja kwa sababu kuna kodi ya wananchi ilipelekwa humo ili kuinua sekta hiyo lakini baadhi ya watu wasio na uzalendo wameamua kuzifanyia biashara pembejeo hizo.

Hivyo aliwataka watanzania kuwa wazalendo na kutoa ushirikiano pindi wanapoona viashiria vya rushwa vinapotokea.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.