• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wajerumani wavutiwa matumizi ya fedha miradi ya maji Mwanza

Posted on: October 4th, 2019

Kamati ya Bunge ya Mazingira, Uhifadhi wa Maliasili na Usalama wa Nyuklia kutoka Ujerumani imeeleza kufurahishwa kwake na namna miradi inayofadhiliwa kwa ushirikiano baina ya Tanzania na Ujerumani inavyotekelezwa.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Ujerumani, Mhe. Sylvia Kotting-Uhl wakati wa ziara ya Kamati yake Jijini Mwanza Oktoba 4, 2019 iliyolenga kutembelea miradi ya maji iliyotekelezwa kwa ushirikiano baina ya Tanzania na Ujerumani.

Aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada na dhamira ya dhati iliyoonyesha kwenye kuwahudumia wananchi wake na alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela kuwa Serikali ya Ujerumani itaendelea kuuenzi ushirikiano huo.

Mara baada ya kutembelea miradi hiyo, Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Bunge la Ujerumani alisema kamati yake imeridhishwa na ilichokiona na alisisitiza kuwa ushirikiano uliyopo baina ya nchi hizo mbili utaendelea.

Awali kabla ya kuwasili Jijini Mwanza, Ujumbe wa Kamati hiyo ya Ujerumani ulitembelea eneo la chanzo cha maji cha mradi wa Simiyu Climate Resilience unaotekelezwa Wilayani Busega, Mkoani Simiyu.

Ikumbukwe kuwa Serikali inatekeleza mradi wa maji wa kimkakati Mkoani Simiyu utakaonufaisha zaidi ya wananchi 800,000 ambao utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 400 kwa kutumia maji kutoka Ziwa Victoria kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mradi huo wa Simiyu utanufaisha Wilaya zote za Mkoa huo na unatekelezwa kwa ushirikiano chini ya ufadhili wa Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maji na Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo ya KfW na Mfuko wa Kijani wa Tabianchi (GCF).

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akiwa ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga waliongozana na Kamati hiyo ya Bunge ya Mazingira, Uhifadhi wa Maliasili na Usalama wa Nyuklia kutoka Ujerumani na walihitimisha ziara yao kwa kutembelea miradi ya majisafi na usafi wa mazingira (majitaka) Jijini Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.