• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wakazi 395 wa Mwanza waishio kwenye miinuko kunufaika na mifumo rahisi ya Maji Taka

Posted on: June 7th, 2022


Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya wanatekeleza Ujenzi wa Mfumo rahisi wa Maji taka kwenye makazi ya miinuko unaotekelezwa Tshs Bilioni 3.8 unaosaidia kuhifadhi maji taka kwenye matanki maalum na kuyatibu badala ya kumwaga kwenye ziwa Victoria kama ilivyokua awali.


Hayo yamebainika leo Juni 07, 2022 mtaa wa Igogo -Sahara wakati wa ziara ya Mhe Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akiambatana na Kamati ya Ulinzi na  Usalama ya Mkoa alipokua akikagua Miradi ya Maendeleo wilayani Nyamaga pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi.


Vilevile, kupitia mradi huo kaya 122 zimeundiwa mfumo wa maji safi na umewezesha ujenzi wa njia maalum za kupanda na kushuka kwenye mitaa hiyo ambapo baada ya ukaguzi wake Mhe Mkuu wa Mkoa ameridhishwa na mradi huo na amewapongeza watekelezaji wa mradi huo wa kisasa wenye ubunifu.


Vilevile, Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza kutoa elimu ya biashara  kwenye vikundi vyote wanavyowakopesha fedha kutoka makundi ya Wanawake, Vijana na wenye ulemavu kwenye Halmashauri hiyo ili kuweka uhai wa vikundi wanavyokopeshwa.


Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo kwenye Mradi wa kikundi cha Vijana watano cha Yuoth Box Media kilichokopeshwa Tshs Milioni 49 mwaka 2021 ambacho kwa sasa kimekuza mtaji hadi kufikia thamani ya Tshs. Milioni 81 huku kikimiliki bidhaa za Habari kupitia Chaneli za mtandaoni za  Yu box Tv na Yu box Studio.


"Hawa wanafanya vizuri ila mimi nimekuja kuona kama kikundi kina afya, je wana taarifa  za mapato na matumizi ya kikundi, wana vitabu vya fedha na wana utaratibu wa kupima maendeleo ya kikundi chao, hapo lazima tujiulize na Maafisa Maendeleo hiyo ndio kazi yetu kuwajengea uwezo", amesema.


Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua Ujenzi wa Barabara ya Hesawa-Yatch Makaburini, Tilapia -Vickfish yenye urefu wa Mita 650 liyotekelezwa kwa zidi ya Tshs. Milioni 348 na ameagiza kurekebisha dosari ndogo kwenye  kingo za barabara hizo na kusafisha mazingira.


Akiendelea na ziara yake Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa pongezi kwa ujenzi wa Mradi wa vyumba 06 vya madarasa kwa mfumo wa ghorofa katika shule ya Sekondari Mkuyuni unaotekelezwa kwa Tshs. Milioni  310 utakaosaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi kutoka 85 hadi 52 kwa darasa kwani madarasa hayo yatachukua wanafunzi 900.


Baada ya kukagua uhai wa Vilabu vya kupambana na rushwa na dawa ya kulevya katika shule ya msingi Nyegezi msafara wa Mhe Mkuu wa Mkoa ulifika kwenye Mradi wa Anuani za Makazi katika Mtaa wa Kisese kata ya Mkolani.


Kabla ya kukagua ujenzi wa jengo la Benki ya CRDB tawi la Buhongwa wenye thamani ya Tshs. Milioni 500, Ujenzi wa Kituo cha Afya Bulale kata ya Buhongwa wenye thamani ya Tshs Milioni 500 umehitimisha ukaguzi wa miradi wilayani Nyamagana ambapo Mhe. Mkuu wa Mkoa amesisitiza ukamilishaji wa mradi huo kwa wakati ili uanze kuwahudumia zaidi ya wananchi elfu 5 wanaokusudiwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.