• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wakazi wa Kisiwa cha Gana Wilayani Ukerewe wapewa Rai ya kufanya kazi ili kujiletea maendeleo

Posted on: November 5th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amewataka wananchi wa Kitongoji cha Gana- Kamasi kufanya kazi kwa bidii na kuacha tabia ya kustarehe wakati wote ili waweze kumudu mahitaji ya familia na kujiletea Maendeleo.

Malima ametoa wito huo leo Novemba 05, 2022 alipofika Kisiwani humo kukagua Ujenzi wa Mradi wa Maji na Zahanati iliyo katika hatua ya Msingi inayojengwa kwa nguvu za wananchi ambayo itawahudumia zaidi ya wananchi Elfu Sita wanaoishi katika kitongoji hicho kilicho kwenye Kijiji cha Kamasi.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara Mkuu wa Mkoa ameiagiza kamati ya Ujenzi wa Zahanati kusimamia ujenzi huo kwa Uzalendo ili wananchi hao wapate huduma za Afya siku za usoni na sambamba na hilo amesema Mhe Rais Samia pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu wamechangia jumla ya shilingi milioni 20 kwenye ujenzi huo.

"Naiagiza kamati ya ya Ujenzi wa Zahanati hii kusimamia ujenzi huu kwa uzalendo ili wananchi wetu wapate huduma za Afya na kuepuka usumbufu kwa kwenda Nansio kwa ajili ya kupata matibabu." Amesema Malima.

Kufuatia Agizo la Mhe. Kassim Majaliwa alilolitoa Oktoba 20 2022 la kumtaka ndani ya siku 15 Mkandarasi Intercounty Co LTD anayejenga Barabara za Kilomita 1 kwa kiwango cha Lami Nyepesi Wilayani Ukerewe ziwe zimekamilika Mhe. Malima amekabidhiwa rasmi Barabara hizo Mjini Nansio.

"Kama mnakumbuka Mkandarasi huyu alikua anasuasua kwenye Ujenzi hadi Mhe. Waziri Mkuu alimuita Dodoma Mkandarasi huyu na baada ya mazungumzo alipewa siku 15 kufikia leo awe amemaliza, nashukuru amekamilisha bado Mambo madogo tu kama taa ambazo ndani ya wiki moja zitawekwa.

Aidha, ametoa rai kwa wananchi kutunza Miundombinu ya Barabara hizo ili ziwasaidie kwa muda mrefu kusafirisha mazao na kuwawahisha kwenye majukumu lakini akawataka kufuata sheria za Barabarani ili kuepukana na ajali.

"Rai yangu kwa Wakandarasi wanaotekeleza  Miradi, naomba sana wawe wazalendo wasipoteze muda na Rasilimali fedha za nchi kwani wakichelewesha miradi wanachelewesha pia Maendeleo ya wananchi." Mhe. Ally Mambile, Mwenyekiti wa CCM (W) Ukerewe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.