• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wakulima waaswa kujiunga vyama vya ushirika

Posted on: September 28th, 2019

Naibu Waziri wa kilimo Hussein Bashe amewatahadharisha wale waliohusika na upotevu wa fedha shilling billion 123 za wakulima kupitia kwenye vyama vya ushirika vya kilimo na masoko ( AMCOS) watachukuliwa hatua za kisheria ili kuurudisha ushirika huo katika mstari na kuhakikisha haki ya mkulima inalindwa.
 
Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa kilimo Hussein Bashe wakati wa mkutano wa 16 wa wadau wa sekta ndogo ya  pamba Tanzania uliowakutanisha wakulima, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, wakurugenzi, wabunge na viongozi vyama vya ushirika kutoka mikoa 17 ya Tanzania bara inayolima zao la pamba ,  uliofanyika jijini hapa lengo likiwa kuongeza tija katika zao hilo hivyo alisema hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wale waliohusika na upotevu wa fedha hizo.

" Hili hatutalifumbia macho kwa sababu  hakuna watu wanaowaibia wakulima kama vyama vya ushirika vya kilimo na masoko (AMCOS ) kwa mujibu wa wakaguzi wa mahesabu ya ndani (COASCO ) kuna upotevu wa fedha za wakulima billion 123  kupitia AMCOS hivyo wale wote waliohusika lazima watachukuliwa  hatua " alisema Bashe.

Pia aliitaka bodi ya pamba nchini kujizatiti na kuimarisha ushirika ili mkulima aweze kuzalisha zao hilo kwa bei ndogo ili aweze kupata tija ya kilimo hicho kwani sekta ya pamba ni nzuri kama utakuwepo muungano wa ushirika utakaofanya mageuzi makubwa hivyo serikali inalenga kuwekeza katika uzalishaji wa mbegu.

Alisema kilimo ni biashara hivyo ni vyema misingi yake iheshimiwe suala la mbegu tayari linashughulikiwa lakini serikali haitakuwa tayari kupewa masharti yasiyokuwa na maslahii kwa Taifa kutoka kwa wafadhili wa nje.

" Serikali itasaidia kupunguza gharama za uzalishaji kwa wakulima na kuwajengea njia nzuri ili wasipate hasara na haitaingilia suala ya bei ya pamba ila soko ndio litakaloamua " alisema Bashe.

Aliongeza kuwa mkopo wa mabenki nchini ni Trillion 16 asilimia nane tu ndiyo inaenda kwenye kilimo, pia sekta ya kilimo haikopesheki kutokana kutokuwa na dhamana hivyo serikali imeamua kutafuta fedha na kuipatia benki ya maendeleo ya kilimo  (TADB) ili ichukuwe dhamana ya kuwakopesha wakulima na imeanza mazungumzo na taasisi za kifedha za kimataifa zitakazoipatia fedha benki hiyo ili iwe na uwezo wa kukopesha wakulima ambapo hivi sasa washapatiwa billion 40.

Awali ya yote akitoa salamu na kumkaribisha mgeni rasmi kufungua mkutano huo wenye kauli mbiu ya wekeza kwenye tija kuongeza kipato cha mkulima na kufikia uchumi wa viwanda Mwenyekiti wa balaza la wakurugenzi bodi ya pamba Joe Kabisa alisema hatari iliyopo sasa katika kilimo cha zao hilo ni uwepo wa funza wekundu hivyo harakati za haraka zinaitajika ili kuwadhibiti ili kuwa na maendeleo endelevu ya sekta hiyo nchini.

Aliongeza kuwa kutokuaminiana ndani ya sekta ni changamoto kubwa inayowakabili hivyo ushirikiano wahitajika ili kusonga mbele pia alimuomba Naibu waziri Bashe kuimarisha mfuko wa pamba unaowezesha upatikanaji wa pembejeo.

Naye Mkurugenzi wa bodi ya pamba Marco Mtunga alisema changamoto muhimu zinazolikabili zao la pamba ni kukosekana kwa uhakika wa upatikanaji wa pembejeo bora zikiwemo mbegu, viuatilifu, mbolea vinyunyizi, utoaji hafifu wa huduma za ugani na matumizi ya zana duni za kilimo hivyo vinachangia tija duni na ubora hafifu.

Dkt Charles Tizeba aliyekuwa Waziri wa Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika, Agrey Mwanri Mkuu wa Mkoa wa Tabora na  Mohammed Yahaya Mkulima ni baadhi ya washiriki wa mkutano huo walisema elimu inayohitajika na yenye maslah kwa taifa ni ya uzalishaji wa zao la pamba .

Pia  ili kuwa na uendelevu wa uzalishaji , serikali iachie mazao makubwa likiwemo zao la pamba yajiendeshe pasipo kutegemea ruzuku ya serikali.

" Uboreshwaji wa viuatilifu uzingatiwe kwa sababu imegeuka changamoto kwa sisi wakulima tunapulizia kwenye mazao yetu lakini mdudu asife na kusababisha tupate hasara"alisema Yahaya.





Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.