• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAKUU WA WILAYA TATU ZA MKOA WA MWANZA WAKABIDHIWA MAGARI MAPYA

Posted on: July 8th, 2024

WAKUU WA WILAYA TATU ZA MKOA WA MWANZA WAKABIDHIWA MAGARI MAPYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Said Mtanda amekabidhi magari matatu mapya kwa ajili ya Wakuu wa Wilaya za Ilemela, Misungwi na Sengerema, yenye thamani ya Tsh. milioni 684 ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na kuleta maendeleo ya Mkoa huo.

Akiongea leo katika hafla fupi ya makabidhiano hayo nje ya viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda amesema anamshukuru Mhe.  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuruhusu na kuidhinisha fedha kwa ajili ya kuwapatia Wakuu wa Wilaya vitendea kazi.

"Sisi Wakuu wa Mikoa nguvu yetu kubwa ni Wakuu wa Wilaya na wao wana maeneo yao ya usimamizi, hivyo ukiwa na viongozi hao hodari na wazuri basi kazi yangu pia itakua nyepesi, hivyo ninawapongeza  wote kwa uchapaji kazi licha ya kutokuwa na vitendea kazi". Mkuu wa Mkoa.

Aidha Mtanda ametoa wito kwa madereva wa magari hayo kuhakikisha wanayafanyia ukaguzi  kila mara baada ya kutembea kilomita elfu 50 na wawapatie taarifa viongozi wao mara baada kufikisha kilometa hizo ili wawaruhusu wakafanye ukaguzi wa magari (Service) hali ambayo itapelekea kuviimarisha vyombo hivyo.

"Na nyie madereva hata kama Mkuu  wako wa kazi atasema tusafiri tu mwambie hapana tufanye service ya gari kwanza , na nyie viongozi wasikilizieni madereva wenu, wakiwaambia gari haiwezi kusafiri msiwalazimishe maana hao ndio wataalamu wa vyombo hivyo". Amesisitiza Mtanda wakati wa makabidhiano hayo

"Msipofanya hivyo mtaisababishia hasara Serikali kwani imetumia na kuwekeza fedha nyingi katika kuwaleteeni ninyi vitendea kazi hivi na nchi hii ina wakuu wa Wilaya wengi ambao bado wana uhitaji wa magari". Mhe.Mtanda

Kadhalika Mkuu huyo wa Mkoa amesema ikiwa tunaelekea katika harakati za uchaguzi, shughuli zitakua ni nyingi kwa Wakuu wa Wilaya zikiwemo za ufuatiliaji, usimamizi, na ukaguzi hivyo amesema atajielekeza pia katika kuhakikiaha Wakuu wa Wilaya za Magu na Ukerewe na wao wanapatiwa vitendea kazi ili kurahisisha utimizaji wa majukumu yao.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya waliokabidhiwa vitendea kazi hivyo, Mhe. Johari Samizi Mkuu wa Wilaya ya Misungwi amesema kwa takribani miaka 3 amekua akitumia gari tofauti  za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi hivyo kupokea gari hiyo mpya itapelekea sasa gari zile alizokua akitumia zikatumike katika shughuli nyingine.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.