• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wakuu wapya wa Wilaya Magu na Ukerewe waapishwa

Posted on: February 3rd, 2023


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigela leo tarehe 03 februari, 2023 amewaapisha Wakuu wa Wilaya za Ukerewe na Magu kufuatia Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania januari 25, 2023.

Akizungumza kwenye hafla ya kuwaapisha Wakuu hao wa Wilaya Mhe. Hassan Bomboko (Ukerewe) pamoja na Mhe Rachel Kasanda (Magu) Mhe. Shigela amewataka kushirikiana na viongozi wengine kusimamia vema masuala ya Utawala bora kwenye maeneo yao kwa kuzingatia namna ya uendeshaji wa taratibu za nchi kwa mujibu wa sheria.

Aidha, amewataka wakuu hao wapya wa wilaya na wale wanaoendelea na majukumu kwenda kusimamia maadili yao binafsi na ya watumishi wa umma katika kuhakikisha mienendo yao katika kuhudumia wananchi inaenda sambamba na utawala bora unaozingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi.

Vilevile, amewataka kwenda kusimamia kwa dhati masuala ya Usalama wa Wananchi kwenye wilaya zao kwa kuhakikisha wananchi wanaishi kwenye Mazingira Safi na Salama kwa Afya za kila siku na kwa kutatua migogoro inayotokana na sekta za Biashara, Uvuvi, Kilimo, Elimu na Miundombinu.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Sixbert Reuben amewapongeza Wakuu wapya wa Wilaya kwa kuaminiwa na kupata Uteuzi na amewaahidi ushirikiano wa dhati kutoka kwenye Chama hicho katika kutimiza majukumu ambayo Mhe. Rais amewaamini na kuwapa jukumu la kutekeleza ndani ya Mkoa wa Mwanza.

"Mmepewa jukumu kubwa sana hivyo nendeni mkafanyeni ziara kwenye maeneo yenu katika kutatua kero za Wananchi ili waondokane na Changamoto zinazowakabili kupitia uongozi wenu na tukifanya hivyo jamii itaishi kwa furaha na itaridhika na ifikapo mwaka wa uchaguzi hakutakua na maswali mengi kwa wagombea wetu." Mhe. Jichabu.

Dkt. Ntemi Kilekamajenga, Jaji mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Mwanza ametoa rai kwa Wakuu hao wapya wa Wilaya kwenda kufanya kazi kwa weledi na kusaidia kutatua migogoro kwa Usuluhishi kwani jambo hilo likienda vema linapunguza kesi mahakamani ambazo pengine zingemalizwa kwenye ngazi za chini.

Ameongeza kuwa, Wakuu hao wa Wilaya wana wajibu pia wa kusimamia kwa dhati Kamati za Maadili za Wilaya kwani wao ndio wenyeviti wa kamati hizo ili kulinda maadili ya Utumishi na kupunguza malalamiko kwenye eneo hilo kutoka kwa wananchi.

"Waheshimiwa Wakuu wapya mlioapa leo nawaomba mkazingatie yote mtakayoahidi Umma na Viongozi waliopo hapa leo na vilevile mkazingatie Maadili yenu ya kazi katika kutekeleza majukumu yenu kwa Mujibu wa Sheria, Kanuni na Maadili." Amesema Jaji Godson Kweka wakati akitoa Kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa Wakuu hao wapya.

Baada ya Kiapo hicho Mhe. Rahel Kasanda, Mkuu wa Wilaya ya Magu amemshukuru Mhe. Rais kwa Uteuzi wake na ametumia wasaa huo kuahidi ushirikiano kwa viongozi na kwamba atahakikisha anafikisha huduma za kijamii kwa wananchi wa Magu na kutekeleza kwa asilimia 100, Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020/25.

"Kwangu mimi Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amenikopesha imani na sina budi kwenda kumuwakilisha kwa Uongozi uliotukuka na nina wajibu wa kutekeleza Ilani ya CCM na ninaahidi kwenda kusimamia haki  kwa Wananchi wa Ukerewe." Amesema, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Mhe. Hasaan Bomboko.

Katika wakati mwingine, Mhe. Shigela amekabidhi Pikipiki 230 zilizotolewa na Serikali kwa Maafisa Ugani mkoani humo na amewataka maafisa hao kwenda kuvitumia vitendea kazi hivyo kuwafikia wananchi ili kuongeza uzalishaji wa chakula.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.