• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waliofuja fedha mradi wa Miyogwezi Ukerewe kuchukuliwa hatua za kisheria

Posted on: July 24th, 2019


Serikali imesema waliohusika kwenye ubadhirifu wa fedha za Mradi wa Umwagiliaji wa Miyogwezi wilayani Ukerewe na kusababisha ujengwe chini ya kiwango na kutokamilika licha ya sh. milioni 750 kutolewa watachukuliwa hatua za kisheria.

Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba alisema jana wilayani Ukerewe baada ya kutembelea na kukagua miradi ya umwagiliaji ya Miyogwezi na Bugorola ambao miundombinu yake imechoka na kusababisha ushindwe kufanya kazi.

Akizungumza kwenye eneo la mradi wa Miyogwezi na wakulima wanaoutumia bonde la mradi huo kwa kilimo, alisema kuna harufu ya rushwa kwenye mradi huo ambao mkandarasi alilipwa sh. milioni 684 kati ya sh. milioni 750 bila kuukamilisha na kuhoji nani alisababisha fedha zikatumika kinyume cha utaratibu wa serikali.

Alisema serikali iliamua kujenga miradi ya umwagiliaji ili kuleta maendeleo endelevu kwenye sekta ya kilimo baada ya kukusanya na kutenga fedha ili wananchi wafaidi keki ya nchi na kulima kwa tija lakini wajanja wa wizara yake wakaleta kampuni za mifukoni zila fedha, kwamba si haki na hawakuwatendea haki watanzania.

Alisema cha kushangaza Ukerewe ilipewa mradi wa miyogwezi na kampuni ya CODA ya nchini Kenya iliyopewa kazi ya kujenga mradi huo ililipwa bila kustahili malipo ya sh. milioni 684 bila kukamilisha mradi huo kwa asilimia 55 baada ya kujenga mabanio mawili chini ya kiwango, magati, mitaro miwili ya maji lakini haikusakafiwa na haikufika mwisho pamoja na vigawa maji 16.

“Siamini nilichokiona hapa na kilichopo kwenye nyaraka (mkataba), mradi huu una harufu ya rushwa na matumizi mabaya ya fedha za umma.Thamani ya mradi ni sh. milioni zaidi ya 700 bado haujakamilika,umetekelezwa kwa asilimia 45 tu.Mkandarasi amelipwa wakati kazi hailingani na thamani ya fedha na waliofanya hayo bado wapo ofisini na kwa nini bado wapo,” alisema Mgumba.

Alionya fedha hizo hazitakwenda bure na kuiagiza Tume ya Umwagiliaji kuandaa taarifa ya kina ya mradi wa Miyogwezi ikiainisha nani alilipwa wakati kazi haikukamilika,waliohusika kwenye ubadhirifu huo, nani aliyesababisha fedha zitumike kinyume cha mipango ya serikali ili ijue njia wanazotumia kutafuna fedha za umma na makosa yasirudiwe.

Naibu Waziri huyo wa Kilimo alisema miongoni mwa kanda ambazo hazikufanya vizuri kwenye miradi ya umwagiliaji ni Mwanza, kwani miradi hiyo ilijengwa chini ya kiwango na kushangaa kwa nini watendaji waliokuwa wakisimamia miradi hiyo bado wako ofisini na kuwataka wajipime kama wanafaa kukalia nafasi hizo.

Mgumba akijibu ombi la wakulima hao la kutaka waletewe fedha zingine baada ya wajanja wakupiga (walikula) fedha za mradi huo alisema serikali haiwezi kuleta fedha hadi ijue nani aliipiga ili achukuliwe hatua za kisheria na liwe fundisho kwa wengine na kueleza kuwa serikali inafanya kazi kwa bajeti iliyopitishwa na bunge.

Aidha, alieleza kuwa wataalamu wanayo kazi ya kuisaidia serikali ili mradi huo wa Miyogwezi ukamilike na itakuwa tayari kutoa fedha baad ya kujiridhisha kuwa fedha za awali zililiwa ndo maana Tume ya Umwagiliaji imeundwa kusimamia miradi ya umwagiliaji.

Awali Mbunge wa Ukerewe (CCM) Josephat Mkundi alisema mradi huo wa kilimo cha umwagiliaji uliokuwa ukisimamiwa na District Agriculture Investment Project (DASIP) ulijengwa mwaka 2013 kwenye kwa ajili ya kuwanufaisha wakulima 194 lakini haufanyi kazi kutokana na miundombinu yake kutokamilika.

Mbunge huyo wa Ukerewe alisema sh. milioni 200 zilitolewa na Dairy Processing & Infrastructure Development Fund (DIDF) ambapo DASIP ilitoa milioni 550 kwa ajili ya mradi huo lakini hadi sasa haujakamilika ambapo akiwa bungeni Januari mwaka huu alihoji serikali ni lini mradi wa Miyogwezi utaboreshwa na kamilika ili kuweza kuwasaidia wakulima wanaotumia bonde hilo kwa kilimo, kulima kwa tija.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.