• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wanafunzi wakutanishwa kufanya mitihani ya kujiandaa

Posted on: August 28th, 2019


Siku chache baada ya Serikali mkoani Mwanza kuweka maazimio 14 kwa  walimu wakuu, maofisa  elimu wa kata na taaluma ili kuinua ufaulu kwa shule za msingi 2019/2020, imeanza kutekeleza kwa vitendo kwa wanafunzi wa darasa la saba wanaotarajia kufanya mtihani wa Taifa kati ya Septemba 11-12, mwaka huu.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Michael Ligola kwa kushirikiana na maafisa elimu taaluma wa wilaya wamelazimika kutunga mtihani unaoelekeana na ule wa taifa na kuwakutanisha wanafunzi wa shule mbalimbali katika kituo kimoja ili kujipima.

Zoezi hilo limeanza ambapo baadhi ya  shule kutoka Jiji la Mwanza na Ilemela zimekutanishwa pamoja  katika Shule ya Msingi Nyanza  na kupatiwa mtihani wa kujipima kwa kufuata muda na masharti yale yale yanayokuwepo katika mtihani wa kitaifa, ambapo shule itakayoifaulisha wanafunzi wengi itakabidhiwa fedha taslimu na  mbuzi kwa ajili ya mahafali.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Ligola, Afisa Elimu Taaluma Mkoa wa Mwanza, Longino Ludovick alisema lengo la Serikali ya mkoa ni kuhamasisha, kuboresha taaluma na kuwaandaa wanafunzi   kuelekea mtihani wa taifa unaotarajia kufanyika Septemba 11 na 12, mwaka huu.

Amwongeza  kuwa kwa  wiki mbili zilizobaki wataendelea na zoezi hilo kwa shule mbalimbali ambapo changamoto zitakazokuwa zikionekana kwa wanafunzi zitatafutiwa majibu haraka kwa kipindi kilichobaki huku akianisha kwamba zawadi zitaanza kutolewa Agosti 30, mwaka huu.


“Leo  kama unavyoshuhudia  tumezikutanisha shule nne ambazo ni Butimba A na B, Bwiru na Gedeli ambazo zimetoka Ilemela na Jiji la Mwanza, hizi shule tumezikutanisha kwa sababu katika mtihani wa Mock zilifanya vizuri hivyo tunataka kuona ipi inaongoza, shule itakayofaulisha wanafunzi wengi watapata zawadi ya pesa na mbuzi  kwa ajili ya kitoweo cha mahafali.


“Kwa wiki moja au mbili zilizobaki tutaendelea katika shule zingine na changamoto zitakazojitokeza tutazifanyia kazi haraka kabla ya mtihani wa taifa, mitihani hii imetungwa na jopo la maofisa elimu kutoka mkoani na wilayani ndio maana unatuona hapa tukishughulika katika kituo hiki cha Shule ya Msingi Nyanza".


Teleza Deus kutoka Shule ya Msingi Gedeli alisema maswali ya somo la Kiingereza waliyopatiwa ni marahisi ambapo aliahidi kupata 45 kwa 50  huku akifafanua kuwa walimu wao wamekuwa wakiwapa majaribio kila ijumaa, hivyo haoni shida kufaulu au shule yao kuibuka kidedea.


Naye Jovin Msiba kutoka Shule ya Msingi Bwiru alisema mtihani huo wa Kiingereza ni kawaida na maswali mengi aliyokutana nayo amefundishwa na walimu. Aliongeza kuwa walimu wao wamekuwa wakiwapatia majaribio  ya kujipima kila wiki ambapo maswali mengi alikuwa anayajua.


Hata hivyo wanafunzi wengine, Julius William na Vailet Javis kutoka Butimba A na B walitamba kwamba shule yao itaibuka kidedea kwani  maswali mengi wamejifunza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.