• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wananchi Nyashigwe Wachinga madawati,kujenga vyumba vya madarasa kwa nguvu zao

Posted on: March 19th, 2021

Wananchi wa Kijiji cha Nyashingwe,Kata ya Chabula wilayani Magu, watengeneza madawati 54,kujenga vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu katika Shule ya Msingi ya kijiji hicho kwa nguvu zao ili kutatua changamoto ya wanafunzi kukaa chini na msongamano darasani.

Madawati hayo 54 yana thamani ya sh.milioni 2.7 huku maboma mawili ya vyumba vya madarasa hivyo ambayo bado hayajapauliwa yakigharimu zaidi ya sh.milioni 6.3.


Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho Devota Aloys alisema jana kwa Mkuu wa Wilaya ya Magu Salum Kalli, wakati akitoa taarifa ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa nguvu za wananchi kijijini humo.


 Alisema kaya sita kila kitongoji za vitongoji vinne zimetengeneza dawati moja ambapo kitongoji cha Nyashigwe kimetengeneza madawati 9 kati ya 11,Kibambu 19 (bado 2), Nyamilomate 20 wanadaiwa moja 1 na Zuli 6 kati ya 8 hivyo madawati 54 kati ya 62 yamepatikana kulingana na mgawanyo wa kila kitongoji.


Aloys alisema madawati hayo yamepunguza uhitaji katika Shule hiyo ya Msingi Nyashigwe yenye wanafunzi 750 kutoka 146 hadi 84,ambapo ina madasara 7 kati ya 17 ili kukidhi mahitaji hivyo madarasa yaliyojengwa na wananchi yakiezekwa yatasaidia.


Pia alisema shule hiyo ina uhaba wa matundu 29 ya vyoo yaliyopo ni 6 kati ya 35 na kuiomba serikali iwasaidie kujenga vya kisasa ili kunusuru afya za wanafunzi na baada ya wananchi kujenga zahanati kwa nguvu zao na kukamilisha boma kwa sh. milioni 8 linahitaji kuezekwa.


Kwa upande wake Kalli alisema serikali lazima iunge mkono juhudi za wananchi na itaendelea kuboresha elimu baada ya kufuta ada kuanzia darsa la awali hadi sekondari kidato cha nne ili watoto wasome hasa wa kike na kwa heshima ya wananchi kwa kazi waliyoifanya atapeleka madawati 10 kwenye shule hiyo.



“Madawati haya yatawanufaisha watoto,elimu ni bure hivyo wazazi waacheni watoto wa kike muache tamaa ya mali, ni tunu katika taifa letu na hapa watatoka makamu wa rais, naibu spika,mawaziri na makatibu wakuu mbalimbali wanawake, kwanza ni waaminifu hawapindishi maneno kama wanaume,”alisema Kalli na kuwataka watoto wawaenzi wazazi na wananchi kwa kufaulu mitihani yao vizuri.


Pia alisema Aprili 30,atapaua na kuezeka vyumba vya madarasa vilivyojengwa na wananchi hao na atamwagiza Meneja wa Tanesco Magu aende kweye shule hiyo kupima nguzo zinazohitajika ili waunganishwe kwenye mradi wa umeme vijijini (REA).

Aidha baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo,waliwashukuru wazazi na wananchi kwa kujitoa kwao na kuwajengea madarasa pamoja na kuwatengenezea madawati.


“Tunawashukuru wazazi kwa jitihada zao, wengi mavazi yalichafuka kwa tulikuwa tunakaa chini, pia tunamshukuru Rais John Magufuli kwa kutoa elimu bure,”alisema Bulala Simba.


Patrick Costantine yeye alisema madawati hayo yatakuwa kichochea cha kusoma kwa bidii ili wafaulu masomo na kutimiza ndoto zao huku Kado Safari akisema kuondolewa kwa changamoto ya kukaa chini wataongeza bidii ya kujifunza zaidi.  


Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Ishengoma Kabuche, alisema uhaba wa madawati na vyumba vya madarasa uliathiri utoaji wa taaluma na kushusha ufaulu, hivyo jitihada na mchango wa wananchi wa kuchonga madawati 54,ujenzi madarasa mawili na ofisi ya walimu kutaondoa msongamano wa wanafunzi darasani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.