• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wananchi wa Kisesa-Kayenze Wilayani Magu kunufaika na Miradi ya Barabara

Posted on: June 3rd, 2022


Leo Juni 03, 2022 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel amekagua ujenzi wa barabara ya Kisesa-Kayenze wilayani Magu yenye urefu wa KM 10 inayogharimu Tshs Milioni 134 kiwango cha Changarawe ambapo amemuagiza Mkandarasi kukamilisha kwa wakati na kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuimarisha mitaro ya maji ili iweze kudumu muda mrefu.


Akikagua Mradi wa Vyumba vinane vya madarasa vilivyotekelezwa kwa Tshs. Milioni 160, Mhe.Mhandisi Gabriel kwenye shule ya Sekondari Lugeye ametoa rai kwa wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii na kufanya mazoezi ya viungo ili waweze kufaulu kwenye mitihani yao.


"Kwanza mtangulizeni Mungu, pili epukeni tabia mbaya ya mahusiano shuleni, someni kwa bidii mtafanikiwa huu ni wakati wa kutengeneza maisha yako tena somo la hesabu lipeni kipaumbele." Mkuu wa Mkoa.


Mwanafunzi Melesiana Sylivester wa Kidato cha nne katika shule ya Sekondari Lugeye ajipatia zawadi ya papo hapo zaidi ya Shilingi elfu 60 kutoka kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa baada ya kujibu vizuri swali la somo la Hesabu alipoulizwa njia zinazotumika kukokotoa 'simultaneous equation'.


Vilevile, Mhe Mkuu wa Mkoa amefanya ziara kwenye Mradi wa Maji ya bomba Kahangara wenye thamani ya zaidi ya Milioni 500 huku ukitarajiwa kuwahudumia zaidi ya watu 9600 ambapo amewapongeza RUWASA kwa utekelezaji wa mradi huo ambao utawapunguzia wananchi umbali wa kutembea kutafuta huduma hiyo na upatikanaji wa maji salama utapanda hadi 86% kutoka %34 za hivi sasa kwenye eneo hilo.

Aidha, Mhandisi Gabriel amekagua mradi wa jengo la X-RAY na Ultra Sound wenye thamani ya Milioni 66.2 katika Kituo cha Afya Kahangara na amesisitiza marekebisho kwenye dosari chache zilizobainishwa ili mradi uwe nadhifu na uweze kutoa huduma bora kwa wananchi.


"Naomba mazingira ya shule hii yawe vizuri na rafiki kwa kutolea elimu kwa watoto wetu, hakikisheni kule nje kote kunakua sawa" Amesema Mkuu wa Mkoa wakati wa kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Msingi Bugomba kwa zaidi ya Milioni 89.

Milioni 90 zinazotekeleza ujenzi wa nyumba 3 za watumishi hospitali ya Magu zimemfikisha Mhe. Mkuu wa Mkoa kwenye mradi huo ambapo ameagiza ukamilishwaji wa kujibana ili fedha hizo ziweze kusaidia kuboresha mambo mengine kwenye mradi huo kama kupata makabati au matanki ya maji kwenye nyumba hizo tatu za mfumo wa pamoja.


Mhe.Mhandisi Gabriel amekagua pia mradi wa kampeni ya Lishe, Ziro Malaria na kampeni ya VVU/UKIMWI katika hospitali ya wilaya Magu na ametoa wito kwa wananchi kula vyakula vyenye lishe bora katika kujikinga na maradhi mbalimbali na kuzingatia usharudi wa kitaalamu kujikinga na maambukizi ya Malaria na VVU/UKIMWI.

Aidha, amebainisha kuwa ni lazima Halmashauri ishiriki kutokomeza Matatizo ya utapiamlo kwa watoto kwa kushirikiana na wataalamu wa masuala ya lishe kwa kupanga na kutoa fedha kwenye sekta hiyo muhimu kwa amendeleo ya ustawi endelevu.

Mradi wa Anuani za makazi umebainisha kuwa Nguzo za Majina ya mitaa na Barabara wilayani humo umefikia zaidi ya asilimia 50 na ndipo Mhe.Mkuu wa Mkoa akatoa wito kwa watendaji wa zoezi hilo kuwa wabunifu ili kutumia Rasilimali chache zilizopo kukamilisha zoezi hilo nyeti.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.