• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WAELIMISHWE VIZURI KUHUSU UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA: M/KITI WA TUME

Posted on: August 9th, 2024

WANANCHI WAELIMISHWE VIZURI KUHUSU UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA: M/KITI WA TUME


Mwenyekiti wa Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wadau kuwaelimisha wananchi ili waweze kushiriki kwenye zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura kama msingi wa uchaguzi bora wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Ametoa wito huo leo Agosti 9, 2024 Mkoani Mwanza wakati akifungua mkutano wa Tume hiyo na wadau uliofanyika uliolenga kupeana taarifa mbalimbali ikiwemo kuandikisha wapiga kura wapya, uboreshaji wa daftari pamoja na hatua za maandalizi kama ununuzi.

"Ndugu wadau, kama nilivyo sema hapo awali nchi yetu inakwenda katika uchaguzi mkuu hapo mwakani, zoezi hili la uboreshaji tayari limezinduliwa mkoani Kigoma Julai 20, 2024 na Mhe.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,huu ni mzunguko wa tatu kwa Mkoa wa Mwanza na Shinyanga utakaoanza Agosti 21 hadi 28 mwaka huu" ,amesema Mhe.Mwambegele

Vilevile amefafanua kuwa ni kosa la jinai kwa mtu kujiandikisha mara mbili kupiga kura na adhabu yake ni kifungo kisichozidi miezi 6 au kisichozidi miaka miwili au faini ya Tshs laki moja au isiyo zidi laki tatu hivyo ni vyema wananchi wakaelimishwa vizuri.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume hiyo ambaye pia ni Katibu wa Tume Bw. Ramadhan Kailima amesema kwa Mkoa wa Mwanza wanatarajia kuwa na wapiga kura wapya 190,131 sawa na ongezeko la asilimia 10.3 la wapiga kura 1,845,816 waliopo sasa.

Makundi mengine yanayoshiriki mkutano huo ni Maafisa Habari ngazi ya mkoa na Halmashauri, wahariri wa vyombo vya habari, vijana, wazee, wanawake, walemavu pamoja na taasisi mbalimbali zinazojihusisha na harakati za maendeleo kwa wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.