• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wananchi Wilayani Magu wahimizwa kushiriki zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

Posted on: July 14th, 2022


Viongozi wa Wilaya ya Magu wametakiwa  kuhakikisha kuwa wananchi wanajiandaa vema katika zoezi la sensa ya watu na Makazi itakayofanyika Agosti 23 2022, huku Elimu kuhusu Sensa imetakiwa kuendelea kutolewa maeneo mbalimbali ili ifikapo mwezi Agosti wananchi wote wawe wamepata taarifa.

Hayo  yamebainishwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe.Dkt.Stergomena Tax wakati akitoa salamu za mwenge wa Uhuru katika viwanja vya Kisasa mapema hii leo.

"Taarifa zote zitakazokusanywa wakati wa Sensa zitakuwa ni kwa malengo ya maendeleo ya Nchi na si vinginevyo niwaombe elimu iendelee kutolewa ili ifikapo Agosti 23 elimu iwe imefika hadi maeneo ya vijijini,"amesema Mhe. Tax.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe.Salum Kalli awali akiwasilisha salamu za Wilaya ya Magu kwa Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Ndugu  Sahili Nyanzabara  Geraruma   amemtaka Kiongozi huyo kumfikishia Salamu za Shukurani Mhe.Rais kwa kuendelea kutuletea fedha za miradi mbalimbali ikiwemo Elimu, Afya,Maji na Miundombinu ya barabara.

Mhe.Kalli ameahidi usimamizi mzuri wa miradi yote na kusisitiza kuwa Mhe.Rais ana imani kubwa na viongozi aliowapa dhamana hivyo wasimuangushe.


"Ndugu Geraruma tupelekee salaam za Shukurani za wana Magu kwa Mhe.Rais kwamba sisi wana Magu tunashukuru sana kwa kuendelea kutuletea fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya yetu, tunaahidi kuendelea kusimamia vema miradi tunayopewa," amesema Mhe.Kalli.

Naye  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Marry Masanja amesema hatawavumilia watendaji kazi wasioendana na kasi ya Mhe.Rais. kwa kuwa Mhe. Rais analeta fedha nyingi sana kwa ajili ya maendeleo hivyo hatuna budi kusimamia kikamilifu.

Naye Mbunge wa Jimbo la Magu Mhe. Destery Kiswaga amewahimiza wananchi wote wa magu kushiriki kikamilifu zoezi la Sensa ili kuiwezesha Serikali kupanga maendeleo kwa kwa kuzingatia idadi ya watu.

Hata hivyo, Ziara ya Mwenge wa Uhuru imeingia katika siku ya tatu mkoani Mwanza katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu ambapo Mwenge wa Uhuru

umezindua miradi 3,kukagua miradi 2 na kuweka jiwe la msingi mradi 1 yote ikiwa na thamani ya shilingi bilioni 1.02 ambapo kesho, Julai 15 itakabidhiwa Wilaya ya Ilemela na utakuwa umekamilisha kilomita 120 tokea ukimbizwe Wilaya ya Magu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.