• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Watano wakamatwa mauaji ya Albino Kwimba,Mwanza

Posted on: November 9th, 2022


Watu watano wakamatwa wakituhumiwa kuhusika na Kifo cha kikatili cha Ndugu Joseph Mathias (28) kilichotokea usiku wa tarehe 02 Novemba, 2022 kwa kukatwa Mkono wa kulia na kusababisha kifo chake katika kijiji cha Ngulla wilayani Kwimba.

Hayo yamebainishwa na Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu maendeleo ya kuwasaka watuhumiwa wa sakata hilo ambao wamekamatwa kwenye maeneo wilayani Misungwi.

"Wiki iliyopita yalitokea mauaji mabaya sana na nilitoa maagizo kwa jeshi la Polisi na vyombo vingine vinavyohusika na uchunguzi kuhakikisha wanawakamata watu wote waliohusika na tukio hilo na juzi wamewakamata wahalifu hao, kwakweli nawapongeza sana Jeshi la Polisi na wananchi wote waliotoa ushirikiano." Amesema Mhe. Malima.

Amefafanua kuwa Marehemu Mathias amefikwa na umaiti kutokana na kupoteza damu nyingi kwani pale nyumbani kwake alikatwa mkono kwa kutumia kitu kikali na marehemu alibaki akihangaika pale na akapoteza damu nyingi sana.

Vilevile, ametoa agizo kwa vyombo vinavyohusika na Uchunguzi kuendelea kufuatilia mwenendo mzima wa uovu huo ili asibaki hata mtu mmoja aliyehusika bila kukamatwa aidha awe aliyetekeleza mauaji, aliyetengeneza mazingira, mwendesha bodaboda aliyewabeba, Mganga wa kienyeji au hata mwanasiasa yeyote kama alihusika.

Kamanda wa Polisi Mkoa SACP Wilbroad Mtafungwa amefafanua kuwa Marehemu Joseph Mathias aliuawa usiku wa tarehe 02 Novemba 2022 na watu waliofika nyumbani kwake na kumwita atoke nje na alipotoka alishambuliwa na takribani watu wapatao watano na kumkata Mkono na kuondoka nao na kusababisha kifo chake kwa kupoteza damu.

Ameongeza kuwa Jeshi la polisi limefanya Msako mkali kwenye maeneo mbalimbali wilayani Kwimba na siku ya Tarehe 06 Novemba, 2022 walifanikiwa kumkamata mtu mmoja aliyebeba begi jeusi na baada ya upekuzi alikutwa na Mkono wa binadamu na mtuhumiwa alikiri kuhusika kwa kushirikiana na wenzake kufanikisha uovu huo.

"Baada ya Uchunguzi wa Kitaalamu imebainika ya kwamba Mkono ule ni wa Marehemu Joseph Mathias na Mtuhumiwa huyo pamoja na wenzake tunaendelea kuwahoji na kwa hakika msako mkali unaendelea na kwamba hatobaki mtu hata mmoja ambaye amehusika na mauaji hayo na baadae watafikishwa mahakamani." Kamanda Mtafungwa.

Kamanda Mtafungwa ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuliamini jeshi la polisi na kusaidia kufanikisha kuwakamata wahalifu na pia ametoa onyo kali kwa jamii kuacha mara moja kufanya vitendo vya kihalifu kwani watakaokaidi agizo hilo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Malima awataka Madiwani kusimamia na kuendeleza vyema rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria

    March 31, 2023
  • RC Malima awahimiza Wana Mwanza kufurika Dimbani Nyamagana Jumamosi hii kuwashangilia wana TP LINDANDA Pamba FC dhidi ya Kitayose

    March 30, 2023
  • Makinda awataka wasomi na wananchi kuyatumia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi kujiinua kiuchumi

    March 29, 2023
  • RC Malima ahimiza kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia

    March 27, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.