• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Watanzania wahamasishwa kula samaki kwa wingi

Posted on: September 25th, 2019


NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema kiwango cha ulaji wa samaki kwa watanzania bado kipo chini sana licha ya taifa kuwa na maziwa, mito, bahari na mabwawa ya wafugaji.

Amesema takwimu zinaonyesha ulaji wa samaki kwa mtanzania ni kilo nane kwa mwaka ukilinganisha mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwamba inapaswa kuwa kilo 20.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Mwanza wakati uzinduzi wa kadi ya Uvuvi jijini Mwanza uliofanywa kati ya Benki ya Posta Tanzania (TPB) na Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (Chakuwata) baada ya kuingia makubaliano ya kukopeshwa pesa ikiwa lengo ni kurasimisha kundi hilo na kuwakwamua kiuchumi.

Ulega alisema anashangazwa kuona kiwango cha ulaji wa samaki kikiwa chini sana licha ya Tanzania kuwa na maziwa,mito, habari na mabwawa ya ufugaji ambapo aliongeza kuwa takwimu zinaonyesha samaki waliovuliwa mwaka jana ni tani 450,000 huku mahitaji ni tani zaidi ya tani 700,000.

“Tangu hafla hii ianze hapa sijaona wavuvi mnacheka au mnafurahi maneno yanayozungumza na viongozi, najua hamu yenu ni kutaka kusikiliza kama Serikali itakuja na tamko mbadala wa kuruhusu mtumie zile nyavu tulizozikataa, pia natambua mnatumia sababu ya kwamba nchi zile za uoande wa pili zinaendelea kutumia nyavu ambazo sisi Tanzania tumezizuia.

“Sheria za makubaliano tulipitisha nchi zote, sasa kama upande wa pili bado hawazingatii sasa tamko letu kama Tanzania sisi tunaendelea kusimamia sheria lakini haitoshi bado tunafuatilia kwa ukaribu kuona kinachofanyika huko upande wa pili, vile vile mkitaka nitangaze leo nyavu zile zitumike itakuwa ngumu kwangu maana zipo taratibu za kubadilidha sheria, hivyo kuweni na imani jambi hilo litakaa sawa.

“Leo tumekutanishwa hapa kwa jambo kubwa sana ambalo tumeona nyinyi wavuvi mnapaswa kuwezeshwa ili kufanya shughuli hii kwa kutumia vifaa vyenye ubora, hivyo Benki ya TPB imekuja hapa kwa ajili ya kuwatambua mtu mmoja mmoja na kikundi, ndio maana mnaingia makubaliano kupitia chama chenu, tunataka kiwango cha ulaji wa sakimi kitoke kilo nane kwa mwaka kifike angalau kilo 20 zinazopendekezwa na WHO,”alisema.

Ulega alisema bado haamini takwimu zinazotolewa kwamba sekta ya uvuvi inachangia pato la taifa kwa asilmia 1.7 ikiwa inashina nagasi ya nne ambapo aliwataka wahusika wa kukusanya takwimu kufanya unyambulisho wa matumizi ya samaki kuanzia minofu yake, mifupa, utumbo, mabondo, matamvua na vitu vingine.

Alisema kitendo cha Benki ya TPB kuingia makubaliano na Chakuwata na kuwakopesha mvuvi mmoja mmoja na kikundi kitawezesha samaki wa kiwango kivuliwa kwa kuwa kutakuwa na vifaa nyenye ubora huku akiweka imani ya kiwango kuongezeka cha ulaji.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TPB, Sabasaba Moshingi alisema ikiwa taasisi za fedha zitasogezwa kwa wananchi, itakuwa ni rahisi taifa kupambana na umasikini na kufanikiwa kukwamua jamii kwa pamoja.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.