• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MABADALA WATAKIWA KUKEMEA VITENDO VYA UKATILI

Posted on: August 28th, 2024

WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MABADALA WATAKIWA KUKEMEA VITENDO VYA UKATILI.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka watoa huduma za afya kwa njia ya tiba asili na tiba mbadala kuhakikisha wanashirikiana na serikali katika kukemea na kuzuia vitendo vyote vya kikatili ikiwemo mauaji ya watoto na wenye ulemavu wa ngozi.

Wito huo umetolewa  leo Agosti 28 wakati akifungua maadhimisho ya siku ya tiba asili ya Mwafrika yanayoendelea katika viwanja vya Furahisha Manispaa ya Ilemela.

Aidha Mhe. Mtanda Amesema waganga wa tiba asili wote wanatakiwa kujisajili kwenye baraza la tiba asili na mbadala na kuhusisha leseni zao kila mwaka ambapo kwa kufanya hivyo watakuwa wakikumbwa na sheria na taratibu za utoaji huduma hizo nchini

"Mimi ninaamini tiba hizi za asili zinapoboreshwa zinafanya kazi sawa na tiba hizi za kawaida na ndio maana Watanzania zaidi ya asilimia 60 nchini wanatumia tiba hizi na zinawasaidia".

Wote tunatambua kwamba tiba asili na tiba mbadala zimekuwa na mchango mkubwa kwa wananchi na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia seksheni ya afya itatoa ushirikiano mkubwa ili kuhakikisha jamii inapata huduma bora". Ameongeza Mhe. mtanda

Naye Makamu Mwenyekiti wa Baraza la tiba asili na mbadala Dkt. Elizabeth Lema amesema waganga wa tiba hizo wametoka kwenye mfumo wa kufanya kienyeji na sasa wanafanya kisasa na wakati mwingine wanatoa huduma jumuishi na wataalamu kutoka hospitali za kawaida ambao wanakiri kwamba tiba za asili zinamsaada mkubwa katika kutibu magonjwa mbalimbali.

Aidha kwa upande wake Kaimu Msajili Baraza la tiba asili na mbadala Bw. Martin Mgogwa amebainisha kuwa baraza hilo pamoja na kuwasajili linasimamia, kuthibiti na kuendeleza tiba asili nchini kwa kuhakikisha kila anayetoa huduma za tiba asili anasajiliwa pamoja na kuhuisha leseni kila mwaka katika eneo lake.

Naye, Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wa Kanda ya Ziwa Bw. John Wanjala ametoa wito kwa wadau kuhakikisha wanafika kwenye ofisi hizo ili dawa wanazotumia ziweze kuchunguzwa kama zina kemikali dawa badala ya kuwa na sumu.

Maadhimisho hayo ya siku ya tiba asili ya Mwafrika yaliyoanza tangu  Agosti 25 mpaka Agosti 31 yanalengo la kusimamia utoaji huduma bora na salama za tiba asili kupitia mifumo sahihi ya udhibiti.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.