• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Watumishi wa kujitolea wakumbushwa kufanya kazi kwa bidii na weledi

Posted on: August 15th, 2022


Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza Joachim Otaru, ametoa rai kwa watumishi wa Afya wanaojitolea kujituma ili kusaidia juhudi za Serikali za kuboresha huduma za afya kwenye maeneo watakayonufaika na mradi wa kuwalipa nusu ya mshahara wa ajira rasmi.

Ametoa wito huo mapema leo Agosti 15 2022 wakati akimwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza kwenye hafla ya Uzinduzi wa mpango wa kujitolea kwa watumishi wa huduma za afya unaoratibiwa na Taasisi ya Mkapa kwa kushirikiana na Serikali utakaowanufaisha watumishi 152 Mwanza na Simiyu.

Vilevile, ndugu Otaru amezipongeza Wizara za TAMISEMl na Afya kwa kupandisha hadhi vituo vya kutolea huduma kutoka Zahanati kuwa Vituo vya Afya au Hospitali za Wilaya na wadau mbalimbali wanaoshiriki juhudi za Serikali za kuboresha huduma za Afya huku akibainisha kuwa mradi huo utasaidia kukuza ujuzi na uzoefu kwa wataalamu hao wakati wakisubiri ajira rasmi.

"Nawapongeza taasisi hii kwa kuamua kutusaidia kupunguza tatizo la upungufu wa wahudumu kwenye sekta ya afya, pia natoa wito kwa mchakato wa kuwapata watoa huduma hizi uzingatie miongozo na taratibu za kiutumishi kwa kupata sifa stahiki nasi tupo tayari kushirikiana nao." Amesema, Katibu Tawala Msaidizi, Utumishi na Rasilimaliwatu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  Mwanza, Daniel Machunda.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Deogratius Kayombo ameishukuru taasisi hiyo kwa kuona tatizo na kuchukua hatua kushirikiana na Serikali kwenye kutatua ama kupunguza Upungufu wa watoa huduma za afya ambao kwa kuanzia mradi huo unatekelezwa kwenye mikoa ya Mwanza, Simiyu, Lindi na Mtwara.

Dkt. Ellen Senkoro kutoka Mfuko wa Benjamin Mkapa amesema kutokana na tatizo la upungufu wa 50% ya watumishi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, taasisi hiyo iliandaa muongozo wa kujitolea kwa Watumishi wa Idara ya Afya ambao ulizinduliwa Septemba 2021 na Waziri wa Afya ukilenga.

Aidha, Dkt Senkoro amefafanua kuwa mpango huo utasaidia kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, Kupambana na maambukizi ya UKIMWI/VVU, huduma za Chanjo ya Uviko 19 na zingin na kwamba taasisi hiyo imeshaajiri watumishi 4159 na Asilimia 50 wamehuishwa kwenye ajira rasmi za Serikali kadiri vibali vya ajira ya afya vinapotolewa na serikali.

Warsha hiyo imewashirikisha Waganga wakuu wa Halmashauri, Maafisa Utumishi wa Mikoa, Makatibu wa Afya, Mashirika yasiyo ya serikali, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wizara ya Afya na wizara ya TAMISEMl.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.