• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mhagama awahimiza Watumishi Sengerema kuongeza bidii kazini wakati Serikali ikiendelea kuboresha maslahi yao

Posted on: February 21st, 2023


Mhe. Jenista Mhagama Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora amewapongeza watumishi wa umma kwa kujituma katika kuwahudumia wananchi na ku yahakikisha wanamsaidia Mhe. Rais kutimiza ndoto ya kuwafikishia watanzania huduma bora katika nyanja zote.

Ametoa pongezi hizo mapema leo februari 21, 2023 wilayani Sengerema alipokua akizungumza na watumishi wa wilaya hiyo akiwa katika muendelezo wa ziara yake Mkoani Mwanza ambapo anakagua miradi iliyo chini ya wizara yake hususani inayotekelezwa na TASAF.

"Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora inashughulikia malimbikizo ya mishahara maana ni haki yao na wenye madai halali wote watalipwa,na zaidi ya Watumishi laki mbili wamepandishwa madaraja ndio maana hivi sasa tunahakikisha mtu akipandishwa daraja anaanza kupata mara moja mshahara wake mpya na hiyo ndio kiu ya Rais Samia katika eneo hili la utumishi." Waziri Mhagama.

Vilevile, amebainisha kuwepo kwa watumishi wa umma wanaoiangusha Serikali na ndio maana kuna ubadhirifu wa fedha za umma pamoja na usimamizi mbovu wa miradi hivyo amewasihi kuwajibika bila kusubiri kusukumwa kuhakikisha wanafanya kazi kizalendo ili kujenga uchumi wa nchi wa wenyewe.

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amempongeza Mhe. Rais kwa kuwajali wanasengerema kwa kutekeleza Miradi ya Kimkakati kama Ujenzi wa Daraja la Kigongo- Busisi ambalo amesema litakapokamilika litasaidia sana kukuza uchumi wa wananchi wa Sengerema na Tanzania kwa ujumla.

Dkt. Angelina Samike, Mjumbe wa baraza Kuu la Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi nchini ametaja changamoto ya uhaba wa watumishi na ametoa ombi kwa Serikali kuendelea kuongeza mshahara ya watumishi ili kuendana na hali ya uchumi kutokana na kupanda kwa bei za bidhaa.

"Tunamshukuru sana Mhe. Rais Samia maana ametuheshimisha wafanyakazi kwa kutupandisha madaraja, kutupunguzia kodi na kuongeza kima cha chini cha mshahara, kutuongezea Mshahara, ametuboreshea mazingira ya kazi kwa kujenga nyumba za watumishi katika sekta ya Elimu na Afya na tunamwombea kwa Mungu afya njema." Amesema,

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.