• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI SAHWA -MWANZA

Posted on: January 23rd, 2026

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 23, 2026 ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kituo cha kusukuma maji na maatenki ya kuhifadhia maji unaotekelezwa katika mtaa wa Sahwa kata ya Lwahnima jijini Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi Mhe. Waziri Mkuu amewataka wakandarasi wanaotekeleza mradi huo kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha unakamilika kwa haraka kwa lengo la kuondoa kero ya maji kwa wananchi, akisisitiza kuwa serikali itakua macho kuwasimamia.

Ameongeza kwa kumuagiza waziri wa maji kuhakikisha kuwa fedha za zinazotoka kwaajili ya miradi ya maji zinakwenda kwenye miradi kwa haraka kwa sababu maji kama huduma ya kijamnii haina mbadala kwa wananchi kutokana na umuhimu wake mkubwa.

Akimkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (MB) amesema atashirikiana na Katibu Mkuu wa wizara yake kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi ili mradi uweze kukamilika ndani ya muda kama mkataba unavyosema.

Awali akisoma taarifa ya mradi Mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira (MWAUWASA) Nelly Msuya amesema mradi huo unaotekelezwa na mkandarasi SINOHYDRO CORPORATION LIMITED & HIGHLAND BUILD CO., LTD (JV) ni sehemu ya programu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Ziwa Victoria (LVWATSAN), yenye lengo la kuboresha huduma ya upatikanaji wa majisafi pamoja na usafi wa mazingira kwa Jiji la Mwanza na maeneo jirani.

Aidha, amebainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kuwanufaisha wakazi zaidi ya 450,000 jijini Mwanza, Magu na Misungwi katika maeneo ya Nyegezi, Mkolani, Buhongwa, Nyamazobe, Nyahingi, Buganda, Luchelele, Lwanhima, Sahwa, Fumagila, Kishiri na Igoma, wakati katika Wilaya za Magu na Misungwi mradi utanufaisha wakazi wa Kisesa, Bujora, Kanyama, Fela na Usagara kwa kupata huduma ya maji safi na ya uhakika, jambo ambalo litachangia kupunguza magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji machafu.

Mradi huo ulianza rasmi kutekelezwa mwezi Juni, 2024 na unatarajia kukamilika mwezi Desemba, 2026 huku gharama za utekelezaji wa mradi huo ni zaidi ya Tsh. bilioni 46.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

    January 26, 2026
  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.