• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Majaliwa akemea Uvuvi haramu nchini

Posted on: November 17th, 2022

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) amewataka wadau na wavuvi kuacha mara moja tabia ya Uvuvi Haramu kwani vitendo hivyo vina madhara makubwa katika Uendelezaji wa sekta ya Uvuvi nchini.

Wito huo umetolewa mapema leo (Novemba 17, 2022) jijini Mwanza na Mhe. Mashimba Ndaki (Mb), Waziri wa Mifugo na Uvuvi kwa niaba ya Mhe. Waziri Mkuu katika Mkutano uliowakutanisha viongozi wa Serikali na wadau wa Sekta ya Uvuvi kutoka Kanda ya Ziwa Victoria uliolenga kuwajengea uwezo dhidi ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji kwa Ukuaji wa Uchumi wa Buluu.

Amebainisha kuwa, Utafiti wa kisayansi uliofanywa mwaka 2021 umeonesha kuwa samaki aina ya Sangara wamepungua kwenye ziwa Victoria kwa asilimia 50 na kwamba wengi wapo kwenye hatari ya kutoweka kutokana na uvuvi haramu na Uharibifu wa mazingira hali inayotishia uwepo wa viumbe hao kwa miaka ijayo.

Aidha, ameelekeza pia Wizara hiyo kuandaa Mikutano ya mara kwa mara ya kuwakutanisha wadau kujadili katika ukuzaji wa sekta hiyo, uboreshaji wa Uvuvi wa samaki wa vizimba kwa kuwaongezea uelewa wanaojihusisha ili kujenga uendelevu na kuwataka maafisa Uvuvi kudhibiti uvuvi haramu kwa kufanya doria ya mara kwa mara.

Vilevile,  Amewaagiza Wizara ya TAMISEMl kusimamia kikamilifu maeneo yenye Rasilimali za Uvuvi, kutenga fedha asilimia tano ya mapato yanayotokana ma sekta hiyo kulingana na miongozo na kamati za Ulinzi za Vijiji na Kata kufanya doria kwa wavuvi haramu na kuwachukulia hatua stahiki.

"Hakuna haki isiyoambatana na Wajibu, Sekta binafsi hakikisheni mnakuza sekta hii kwa kufuata sheria za uvuvi na kwenye vikundi vyenu jiimarisheni kwenye uhamasishaji wa uendezaji wa uvuvi mkubwa ili kukidhi mahitaji ya viwanda na vilevile epukeni kuchakata samaki wachanga kwani tabia hiyo inamaliza samaki ziwani. " Waziri Mkuu.

Hata hivyo, ametoa wito kwa wavuvi kufanya shughuli zao kwa kuzingatia sheria na kanuni ili pamoja na kufanya uvuvi unaokubalika waweze pia kuhifadhi mazingira ya mazalia ya viumbe hai wanaopatikana kwenye bahari, maziwa makuu na madogo na kufanya kuwa endelevu ili kuchochea biashara ya uvuvi.

Awali, amesema kuwa katika mwaka 2021 zaidi ya wananchi Laki moja na elfu Tisini na Moja walijishughulisha moja kwa moja na shughuli za uvuvi na kwamba asilimia 53 wametoka kwenye ukanda wa ziwa Victoria hivyo mchango wa ziwa hilo ni mkubwa sana ambapo wadau wote wanalazimika kuendelea kulinda rasilimaji hiyo muhimu kwa pamoja.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdalah Ulega (Mb) amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 katika ukanda wa Afrika zenye utajiri mkubwa wa maji ambayo ni fursa kubwa ya kukuza uchumi wa wananchi kupitia shughuli za uvuvi na kwamba inachangia Pato la Taifa kwa asilimia 1.8.

"Ziwa victoria pekee lina takribani tani milioni 3 za samaki na maji ya kitaifa ya bahari ya Hindi yanakadiriwa kuwa na Mazalia ya zaidi ya tani laki 1 na hivyo wavuvi wadogo huchangia takribani zaidi ya asilimia 93 na wavuvi wadogo zaidi ya laki moja wamejihusisja moja kwa moja kwenye uvuvi kupitia maji ya asili." Amesema Mhe. Ulega.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amebainisha kuwa wananchi zaidi ya Milioni moja na nusu mkoani humo wanajihusisha na shughuli za Uvuvi ambapo sekta hiyo imekua ikitoa mchango mkubwa sana kwa wananchi hao kwa kuwapatia ajira, uchumi na kipato cha kila siku.

Aidha, amebainisha kuwa Mkoa huo unaendelea kusimamia kikamilifu Ukusanyaji wa mapato kwenye sekta hiyo ili kusaidia ukuzaji wa uchumi wa nchi kupitia sekta hiyo nyeti kwenye ukanda wa Ziwa Viktoria ili kufikia malengo ya kukusanya Bilioni 5.6 kwa mwaka 2022/23.

"Sekta ya Uvuvi imeendelea kuwa chanzo kikuu cha mapato kwa Halmashauri zinazozunguka ziwa Victoria. Mathalani katika mwaka 2021/22 kiasi cha Bilioni Tatu na Milioni Mia nne zilikusanywa na Halmashauri za Mkoa wa Mwanza kutokana na ushuru wa mazao ya uvuvu, leseni za Uvuvi na vyombo vya uvuvi." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi Dkt.Rashid Tamatamah aliwasilisha Changamoto kadhaa zinazoikabili sekta hiyo kuwa ni pamoja na Upungufu wa Mazao ya Uvuvi, Uvuvi haramu, Utoroshaji wa Mazao ya Uvuvi pasipo kulipia Kodi na Uharibifu wa Mazingira na akatumia wasaa huo kukemea vitendo hivyo pamoja na hali ya kipato duni inayowakabili.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. July 29, 2022
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2022 July 03, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI ICAP October 21, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC Malima awataka Madiwani kusimamia na kuendeleza vyema rasilimali za Bonde la Ziwa Victoria

    March 31, 2023
  • RC Malima awahimiza Wana Mwanza kufurika Dimbani Nyamagana Jumamosi hii kuwashangilia wana TP LINDANDA Pamba FC dhidi ya Kitayose

    March 30, 2023
  • Makinda awataka wasomi na wananchi kuyatumia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi kujiinua kiuchumi

    March 29, 2023
  • RC Malima ahimiza kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia

    March 27, 2023
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 33180, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras.mwanza@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.