• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Silaa ampongeza RC Makalla kwa kusimamia na kutatua migogoro ya ardhi Mwanza

Posted on: December 5th, 2023

Waziri Silaa ampongeza RC Makalla kwa kusimamia na kutatua migogoro ya ardhi Mwanza


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa yupo kwenye ziara fupi Mkoani Mwanza na kumpongeza Mkuu wa Mkoa huo Mhe.CPA.Amos Makalla kwa kusimamia na kutatua vyema migogoro ya ardhi ambayo imekuwa kero kubwa kwa wananchi.

Akizungumza leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na watumishi kutoka sekta ya ardhi, Mhe Silaa ameweka bayana kuwa huo ni mfano wa kuigwa kwa watumishi waliopewa dhamana ya kusimamia eneo hilo kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi  na kuzingatia sheria za ardhi.

"Migogoro mingi inaonesha dhahiri chanzo ni sisi baadhi yetu tunaopindisha taratibu zilizopo kwa tamaa binafsi na kuwaacha wananchi wakitaabika na kudhulumika, hilo kama Waziri mwenye dhamana sitalifumbia macho,"amesisitiza Waziri Silaa wakati akizungumza na watumishi kutoka taasisi zilizo chini ya Wizara yake na wengine kutoka Halmashauri.

Amesema Mhe.Makalla amelazimika kutoka ofisini na kwenda kujionea kero zinazowarudisha nyuma kimaendeleo wananchi wake na kuzitolea maamuzi, nyingi zikiwa ni migogoro ya ardhi inayosababishwa na baadhi ya watumishi waliokosa nidhamu ya kazi na badala yake kukimbilia kujinufaisha

"Haiwezekani sheria ziwekwe halafu wengine wanazitii na baadhi kuzipuuzia tena kwa kukusudia huo siyo utaratibu unaokubalika na nitahakikisha uzingatiaji wa sheria za nchi unaheshimika,"Silaa

Waziri Silaa ametoa maagizo kwa kamishna msaidizi wa ardhi Mkoa wa Mwanza Bi.Happines Mtutwa kuhakikisha mkazo wa elimu,ufuatiliaji,na utatuzi wa kero kwa wananchi unafanyika mara kwa mara

Awali kabla ya kikao hicho Waziri Silaa alipata wasaa wa kupata taarifa fupi za mkoa wa Mwanza hasa masuala ya ardhi kutoka kwa mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi anaye kaimu nafasi ya Mkuu wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.