Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana ametoa wito kwa Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wizara zingine kuwajengea uwezo vijana na kuwapatia maeneo ili waweze kufanya kilimo hususani cha Biashara.

Ametoa wito huo mapema leo Februari 16, 2026 wakati akizungumza na timu ya Uhamasishaji wa Kisera kuhusu ukuzaji na uendelezaji wa ushoroba wa Kilimo waliofika ofisini kwake kujitambulisha kuelekea mkutako mkubwa unaotakiwa kufanyika mkoani humo.

Amesema programu nyingi nchini zinaishia kwenye makaratasi jambo ambalo linakwamisha juhudi za serikali za kuwezesha makundi kujihusisha moja kwa moja na kilimo hivyo ni wakati sasa wa kubadili mbinu kwenda kwenye utekelezaji.

Ameongeza kuwa Wizara ya Kilimo inaweza kushirikiana na TAMISEMI kuyatwaa maeneo kutoka kwa wamiliki na kuweka miundombinu ya umwagiliaji na kuhakikisha mikopo kwa vikundi inakwenda kwenye utekelezaji wa kazi zenye tija.

“Programu kama hizi zitusaidie kuwezeaha mamlaka za Serikali za Mitaa kuandaa maeneo kwa wananchi na kuyafanya kuwa dira ya kufanyia biashara kama ni kwa kilimo au ufugaji na uvuvi ili kusaidia vijana wengi ambao hawana ajira.” Balandya.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Agriculture Growth Corrifors if Tanzania (AGCOT) Bi. Elizabeth Musokia amesema kwa muda mrefu Shirika hilo wamekua na wakisimamia Uratibu wa Mpango kazi kwa kushirikiana na wizara zingine ili kuhakikisha kilimo wanakikuza nchini.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.