• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZAIDI YA MILIONI 900 ZA TASAF ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI IGOGWA- ILEMELA

Posted on: February 22nd, 2024

ZAIDI YA MILIONI 900 ZA TASAF ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI IGOGWA- ILEMELA


*Miradi 12 kati ya 20 ya Miundombinu Ilemela yatekelezwa shuleni hapo*


*Watoto wapata shule jirani na mitaa wanayoishi*


*Yasaidia kupandisha mahudhurio ya wanafunzi darasani*


*Jamii yapewa wito kutunza miundombinu ya Shule hiyo*


Siku ya tatu ya kikao kazi kilichowakutanisha waratibu wa TASAF, wahasibu, Maafisa manunuzi na Maafisa ufuatiliaji kutoka Wilaya za Mkoa wa Mwanza imewafikisha timu hiyo kwenye mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Igogwa wilayani Ilemela inayotekelezwa kwa zaidi ya Milioni 900.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa mradi huo Mratibu wa Mpango wa TASAF wa Manispaa ya Ilemela Leonard Robert amesema katika ujenzi wa shule hiyo kuna utekelezaji wa miradi 12 ya Miundombinu kati ya 20 inayotekelezwa kwenye Manispaa hiyo kwa zaidi ya Bilioni 1.9.

Robert amebainisha kuwa pamoja na ujenzi wa jengo la utawala, madarasa 4, maabara za sayansi 2, maktaba, nyumba ya walimu ya familia 2, mabweni 4 pamoja na miundombinu ya maji, mradi huo umepata pia samani kwenye maeneo ya mradi.

"Tunamshukuru Rais Samia kwa kuelekeza zaidi ya Milioni 908 kutujengea miundombinu ya shule yetu ambayo inahusisha madarasa, maabara za sayansi, mabweni, nyumba ya Walimu lakini sio hayo tu bali watoto 40 wamepata pia ufadhili chini ya mradi wa TASAF," amesema Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Athanas Manyika.

Vilevile, Mwalimu Manyika amebainisha kuwa awali watoto walitembea zaidi ya KIlomita 20 kwenda na kurudi kupata elimu kwenye shule ya Sekondari Shibula lakini kwa sasa wamepata shule jirani na mitaa inayozunguka shule hiyo mpya na kufanya mahudhurio ya wanafunzi darasani kuwa mazuri.

Aidha, amebainisha kuwepo kwa juhudi za dhati zinazofanywa na Halmashauri katika kuhakikisha wananchi wanapata fidia ya ardhi kwenye eneo hilo ili kuongeza eneo la shule na kufanya shule hiyo kuwa kwenye mazingira nadhifu na salama wawapo shuleni na bwenini.

Naye, Bi. Anastansia Mpanda, Mtendaji wa  mitaa ya Igongwa na Kimanilwentemi amesema wananchi wanaitiilkia wito na wanachangia nguvu kazi kwa ari kwenye ujenzi na kwamba wanaishukuru Serikali kwa kuwaletea miradi ya jamii.

Halikadhalika, Mwenyekiti wa mtaa wa Igogwa James Kavera amebainisha kuwa wananchi wa mtaa wake wamekua bega kwa bega kwa Serikali kuhakikisha wanachimba msingi, wanasomba maji na mchanga kwenye msingi ili kuwa sehemu ya utekelezaji wa mradi huo.

Mgawa Maswa, Mgane anayelea watoto wanne ameishukuru Serikali kwa kujenga shule ya Sekondari na amebainisha kuwanufaisha watoto wake na wengine kupata fursa ya elimu na hakuacha mbali mradi wake wa ufugaji mbuzi unaoimarishwa kupitia fedha za uhaulishwaji kutoka TASAF.

Ziara ya wataalam hao wilayani Ilemela imehitimishwa kwa timu kuzungumza na walengwa wa TASAF kwenye mtaa wa Igogwe katika kata ya Igogwe ambapo wanufaika hao kwa pamoja wameishukuru Serikali kwa kuwaletea mradi wa shule pamoja na miradi mingine ya huduma za jamii.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.