• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Zaidi ya Wakazi 5000 Buchosa Wilayani Sengerema kupata Maji Safi na salama

Posted on: June 8th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel leo tarehe 08 Juni, 2022 amekagua Mradi wa Maji Magulukenda uliotekelezwa na Wakala ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa Tshs Milioni 150 katika Halmashauri ya Buchosa.


Akizungumza na viongozi baada ya kukagua Mradi huo uliowaondolea adha ya kupata maji mbali wananchi 5151 wa kijiji cha  Magulukenda, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa RUWASA na Halmashauri kutoa elimu kwa jumuiya ya watumia Maji pamoja na jamii inayozunguka Mradi huo ili waumiliki na kuutunza kizalendo uweze kuwasaidia kwa muda mrefu na kupunguza upotevu wa Maji.

"Serikali inaleta fedha nyingi sana tunaunda Jumuiya za watumia maji ili watunze Miundombonu hii hivyo tujiandae kwenye mazingira hayo na tuwe na taarifa ya mapato na matumizi kwa kufuata taratibu za kifedha maana vifaa vinaharibika wakati mwingine na kuhitaji matengenezo, tuweke akiba." amesisitiza.


Awali akiwasili kwenye Halmashauri hiyo, Mhe Mkuu wa Mkoa alikagua Kituo cha Mafuta cha Bulunda-Bukokwa kilichojengwa kwa Tshs. Milioni 220 na kusaidia wananchi kupata huduma hiyo jirani tofauti na awali ambapo walipata umbali wa KM 30 na amewataka viongozi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha mwekezaji huyo ana nyaraka ikiwa ni pamoja na hati ya kiwanja.


Wananchi wa Sukuma-Bukokwa wanaojengewa barabara ya KM 12.5 na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) yenye thamani ya zaidi ya Milioni 200 ambayo imefikia asilimia 50 ya ujenzi wake walifikiwa na ziara hiyo na Mhe Mkuu wa Mkoa amemtaka Mkandarasi kuongeza nguvukazi kwenye ujenzi huo ili kukabiliana na changamoto ya mwenendo wa taratibu wa ujenzi.


Kabla ya Mkuu wa Mkoa kuwapa hamasa ya kufanya kazi kwa bidii Vijana wa kikundi cha 'Vijana na Maendeleo Nyehunge' kilichokopeshwa Tshs Milioni 6 na Halmashauri kwa shughuli za kufyatua Matofali, alikagua Maabara za Masomo ya Sayansi kwenye Shule ya Sekondari ya Nyehunge.


Pamoja na kukagua Mradi wa kampeni ya Lishe, Ziro Malaria na kampeni ya VVU/UKIMWI, Jengo la huduma ya dharula kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa linalotekelezwa kwa Tshs Milioni 300 limehitimisha ziara ya Mhe Mkuu wa Mkoa ambapo Dkt Rajab Amour Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo amebainisha kuwa litakapokamilika litasaidia kupunguza vifo kwa asilimia 40 kutokana na mfumo utaofungwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.