• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 23 WA KATA YA KAGUNGULI UKEREWE WAPATA MAJI SAFI

Posted on: October 8th, 2024

ZAIDI YA WANANCHI ELFU 23 WA KATA YA KAGUNGULI UKEREWE WAPATA MAJI SAFI


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava amezindua mradi wa maji Bukindo- Kagunguli (Tanki la Maji Kagunguli) wenye  thamani ya Tshs. Bilioni 2.3 chini ya usimamizi wa wakala wa maji na usafi wa mazingira mjini na vijini (RUWASA).

Akizungumza na wananchi baada ya uzinduzi wa mradi huo leo Oktoba 8, 2024 uliojengwa na mkandarasi Otonde construction co ltd. Ndugu Mnzava amewataka wananchi kulinda miundombinu ya mradi huo ili uweze kuwasaidia kwa muda mrefu.

Aidha, kiongozi huyo ameiagiza jumuiya ya watumia maji kuhudumia wananchi kwa haki na usawa kwa kuzingatia bei ya maji inayoweza kuhimilika na mwananchi mwenye kila hali ya uchumi ili malengo ya kuipatia jamii maji safi na salama yatimie kwa wote.

"Naomba tuutunze mradi wetu na miundombinu yake ili iweze kutuhudumia kwa muda mrefu na tusimvumilie mtu atakayetaka kuhujumu lakini pia jumuia ya watumia maji siku zote tuhudumie jamii kwa usawa na haki kwenye bei kwa kuhakikisha inakua rafiki kwa wote."

Awali, Kaimu Meneja wa RUWASA wilaya ya Ukerewe Mhandisi Flowin Mkechi amesema mradi huo unahusisha matenki mawili ya maji yenye ujazo wa lita 150,000 na kwamba wananchi elfu 23.2 kutoka kwenye vijiji vya Buzegwe, Nampise, Muhande na Buguza katika kata  ya Kagunguli vimefikiwa na mradi huo.

Halikadhalika, kiongozi huyo wa mbio za mwenge mwaka huu amemkabidhi Bi. Khadija Nyankubi nyumba ya kisasa aliyojengewa na wadau kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa huo la kumpatia zawadi bibi huyo mzalendo aliyetoa eneo la ujenzi wa mradi huo bila kudai fidia.

Katika wakati mwingine, Mwenge wa Uhuru wilayani Ukerewe umezindua mabweni 3 ya kidato cha V na VI, madarasa 8 na matundu 33 ya vyoo vyenye thamani ya tshs. Milioni 694.2 katika shule ya sekondari Bukondo ambapo Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Emanuel Bomba ameishukuru Serikali kwa miundombinu hiyo.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.