• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZIARA YA RC MTANDA HOSPITALI YA JESHI YAWAIBUA WANANCHI, WAFIKA KUPATA HUDUMA ZA KIBINGWA

Posted on: June 4th, 2024

ZIARA YA RC MTANDA HOSPITALI YA JESHI YAWAIBUA WANANCHI, WAFIKA KUPATA HUDUMA ZA KIBINGWA


Kufuatia ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda aliyoifanya Mei 24, 2024 kukagua huduma mbalimbali zinazotolewa na Hospitali ya Kanda ya Jeshi la Wananchi Mwanza iliyopo wilayani Ilemela, wananchi waanza kufika ili kupata matibabu ya kibingwa na kupongeza kwa huduma nzuri.

Hayo yamedhihirika baada ya Bi. Dina Mgeta kutoka Mkoani Mara kufika kwenye hospitali hiyo mnamo Mei 31, 2024 akiwa na uvimbe usio wa kawaida shingoni ili kupata matibabu ambapo leo Juni 04, 2024 mgonjwa huyo amezungumzia furaha yake baada ya kufanyiwa upasuaji wenye mafanikio na hali yake kuwa nzuri.

Mgonjwa huyo amemshukuru Mkuu wa Hospitali hiyo kwa ukarimu na moyo wa kiungwana kwani mara tu baada ya kumpokea alihakikisha anamhudumia hata baada ya kubaini kuwa mgonjwa huyo aliyeletwa na mama yake mzazi kutokua na fedha za matibabu wala bima ya afya hivyo kulazimika kuomba kupatiwa matibabu kwa msamaha.

Mgonjwa huyo ameonesha furaha yake kutokana na kupata matibabu mazuri ya kibingwa na akatumia wasaa huo kutoa wito kwa wananchi wengine kuhakikisha wanakata Bima ya Afya kwani inasaidia sana endapo unapata maradhi na kuhitaji matibabu jambo ambalo yeye alishindwa kufanikisha kutokana na kukosa bima.

Mkuu wa Hospitali ya Kanda ya Jeshi Mwanza ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Upasuaji na ndiye aliyemfanyia Upasuaji mgonjwa huyo, Luteni Kanali Ahmed Shabhay amesema walimpokea mama huyo akiwa na uvimbe mkubwa shingoni (Huge Multi-nodular Goiter) na alihitajika kufanyiwa upasuaji wa kutoa uvimbe huo.


Amesema, Mama huyo hakuwa na fedha za matibabu na wala hakua mnufaika wa bima ya afya na aliifikisha changamoto yake kwenye uongozi wa hospitali nao kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa walifanikisha na kumfanyia upasuaji Mei 31,2024 ambao umeenda salama kutokana na vifaa tiba na wataalamu tiba na kwamba kwa sasa yupo salama na ameruhusiwa kwenda nyumbani kwani matibabu hayo yamekamilika.

Luteni Kanali Ahmed Shabhay ametoa wito kwa wananchi kutoka Mwanza na mikoa ya jirani kufika kwenye hospitali hiyo kupata matibabu ya kibingwa kwani wana watoa huduma wabobevu na vifaa vya Kisasa na kwamba wanahudumia Maafisa, Askari na familia zao pamoja na raia kwa njia zote za malipo ya papo kwa papo na Bima ya afya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.