• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Akamatwa kwa kuwatapeli Wana CCM

Posted on: June 6th, 2019

Askari wa jeshi la magereza,Kibemba Warioba (27) mwenye namba B.9205 WDR amekamatwa na jeshi la polisi mkoani Mwanza  kwa kosa la kuanzisha saccos ya info tell CCM na kuwatapeli wanachama wa chama cha mapinduzi(CCM).

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Mwanza,Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo,Jumanne murilo alisema askari huyo alikamatwa juzi baada ya kupokea malalamiko ya wanachama wa CCM kwamba kuna saccos ya info Tell CCM inatoa gawio zuri na kubadili maisha haraka ya wanachama.

Kamanda Murilo alisema baada ya taarifa hiyo kupokelewa, askari wa Mwanza walishirikiana na askari wa Mkoa wa Kagera walifuatilia mwanzilishi wa saccos hiyo na kufanikiwa kumkamata askari huyo wa magereza akiwa na  laini za simu tano zikiwa zimesajiliwa kwa majina tofauti tofuati.

 “Mtumishi huyo ameichafua sura ya jeshi la magereza, serikali, amechafua jina la chama cha  CCM, hatuwezi kuvumilia watu wa aina hii kuendelelea kufanya uhalifu na utepeli, tutawashughulikia na kama kuna watu wenye nia ya kujihusisha na shughuli isiyo halali ni vema wakaiacha,”alisema.

Alisema baada ya uchunguzi dhidi ya askari huyo wa magereza alikiri ndiye mhusika na tayari amewatapeli wanachama wa CCM wengi na watu wengine wa kawaida  huku akitambulisha kwa vyeo mbalimbali  vilivyopo ndani ya CCM na serikali.

 “Shughuli hii si kwamba alikuwa anaifanya yeye mwenyewe bali na watu wengine na baadhi tumewakamata ambao wamewatapeli wanachama wa CCM wakiwaeleza kuwa watapata gawio zuri na maisha yao yatakuwa mazuri na bora”alisema Murilo.

Hata hivyo Kamanda Murilo aliwataka wanachama wa CCM na watu wengine ambao wametapeliwa na saccos ya Info Tell CCM kufika katika vituo vya polisi kutoa taarifa zao ili waweze kurejeshewa fedha zao na hata kutoa ushahidi pale mtuhumiwa atakapofikishwa mahakamani.




Wakati huo huo watu 29 wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa makosa mbalimbali yakiwamo mauaji ya wavuvi, wizi, unyang’anyi na upatikanaji wa dawa za kulevya aina ya bangi na mirungi.

Kamanda Murilo alisema miongoni mwa watuhumiwa hao, wapo watu wawili ambao  ni wavuvi wamekamatwa kwa tuhuma za mauaji  katika kisiwa cha Ukara baada ya kuwavamia wavuvi  wenzao wawili ambapo waliwafunga kamba miguuni na mikononi na kuwatumbukiza ziwani.

Alisema katika tukio hilo, mvuvi mmoja kati ya wale waliofungwa kamba aliweza kupoteza  maisha  huku wavamizi wakiwapora  injini ya boti, kokoro moja la dagaa, tanki la mafuta, simu na vitu mbalimbali vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya sh milioni tano.

Vile Kamanda Murilo alisema katika operesheni ya juzi mkoani Mwanza, polisi walifanikiwa  kuwakamata watu watano kwa kosa la kupatikana na vifaa vya kutengeneza noti za fedha bandia  za Tanzania na dola ya Marekani.





Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.