• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

Posted on: January 8th, 2026

Bodi ya Barabara Mkoa wa Mwanza imetakiwa kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara kwa kuhakikisha inazingatia ubora unaoendana na thamani ya fedha zinazotolewa na Serikali.

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 08 Januari 2026 na Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Christopher Ngubiyagai alipokuwa akifungua Kikao cha Kwanza cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Mwanza kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Mhe. Ngubiyagai amesema ili kufikia malengo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta ya miundombinu, hususan kuhakikisha barabara zote nchini zinapitika katika vipindi vyote vya mwaka, ni lazima watendaji kubadili fikra, kuongeza uwajibikaji na kufanya kazi kwa kujituma zaidi.

Amesisitiza kuwa vikao vya bodi vinapaswa kuwa chachu ya kutatua changamoto zilizopo badala ya kuwa majukwaa ya majadiliano pekee, akihimiza utekelezaji wa maamuzi yanayofikiwa.

“Kupitia vikao vya bodi tuhakikishe tunapokea na kujadili changamoto zilizopo, na baada ya kikao kila mmoja akasimamie utekelezaji wa maazimio ili wananchi wanufaike kwa kusafirisha mazao yao na kutumia barabara kwa usalama”. Amesema Mhe. Ngubiyagai.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo ameihoji bodi hiyo juu ya kuchelewa kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Sengerema–Nyehunge licha ya mkandarasi aliyeshinda zabuni hiyo kusaini mkataba.

“Mkandarasi tayari amesaini mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo lakini bado hajaanza kazi. Ni lini ataanza ujenzi maana wananchi wanateseka kutokana na mashimo mengi yaliyopo kwenye barabara hiyo”. Amehoji Mhe. Shigongo.

Akijibu hoja hiyo, Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mwanza Mhandisi Pascal Ambrose amesema Serikali inatarajia kumlipa mkandarasi huyo malipo ya awali, hatua itakayomwezesha kuanza utekelezaji wa mradi huo hivi karibuni.

Amesema ujenzi wa barabara hiyo ni miongoni mwa miradi muhimu itakayosaidia kuboresha usafiri, kuchochea shughuli za kiuchumi na kupunguza kero kwa wananchi wa maeneo yanayohudumiwa na barabara hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.