• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BVR KITS 4,257 KUBORESHA DAFTARI SHINYANGA NA MWANZA

Posted on: August 20th, 2024

BVR KITS 4,257  KUBORESHA DAFTARI SHINYANGA NA MWANZA

Jumla ya BVR Kits 4,257 zimesambazwa mkoani Mwanza na Shinyanga kwa ajili ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linalotarajiwa kufanyika kwenye mikoa hiyo kuanzia kesho tarehe 21 hadi 27 Agosti, 2024.

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Asina Omari amesema hayo mkoani Mwanza leo tarehe 20 Agosti, 2024 na kuongeza kuwa kati ya BVR Kits hizo 3,590 zitatumika vituoni na 667 ni za akiba.


“Jumla ya watendaji 7,562 watahusika katika kuendesha zoezi hilo kwa mikoa hii ya Mwanza na Shinyanga, idadi hiyo inajumuisha Waratibu wa Uandikishaji wa Mikoa, Maafisa Waandikishaji ngazi ya Halmashauri, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Halmashauri, Maafisa Waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata, Waendesha vifaa vya Bayometriki na Waandishi Wasaidizi,” amesema.


Ameongeza kuwa kutokana na takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 400,082 kwenye mikoa hiyo.


“Mkoani Shinyanga wapiga kura wapya wanaotarajiwa kuandikishwa ni 209,951 na mkoani Mwanza wapiga kura wapya 190,131 wataandikishwa ambapo kwa ujumla wapiga kura wapya watakaoandikishwa ni 400,082,” amesema.


Ametoa wito kwa wananchi wa mikoa hiyo waliotimiza umri wa miaka 18 na wale watakaotimiza umri huo ifikapo tarehe ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 na wanaohitaji kuboresha taarifa zao  kujitokeza mapema na kuacha kasumba ya kusubiri siku ya mwisho.


Uzinduzi wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ulifanyika mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2024 ambapo ulienda sambamba na kuanza kwa mzunguko wa kwanza wa uboreshaji kwenye mikoa mitatu ya Kigoma, Tabora na Katavi na kufuatiwa na mzunguko wa pili ambao umejumuisha mikoa ya Geita na Kagera.


Kwenye zoezi hilo vituo vya kuandikisha wapiga kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.