• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DC LUDIGIJA ATOA WITO WIZARA YA MIFUGO KUSIMAMIA NA KUFUATILIA DAWA ZA MIFUGO

Posted on: August 6th, 2024

DC LUDIGIJA ATOA WITO WIZARA YA MIFUGO KUSIMAMIA NA KUFUATILIA DAWA ZA MIFUGO


Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija ametoa wito kwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuweka Kitengo maalumu cha ufuatiliaji na usimamizi wa dawa ya mifugo kama ilivyo kwa dawa za binadamu na vipodozi ili kuleta ufanisi katika uuzaji wa dawa za mifugo.

Mhe. Ludigija ametoa wito huo alipotembelea mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Agosti 06, 2024 katika viwanja vya Nyamhongolo yanapofanyika maonesho ya nanenane kwa Kanda ya Ziwa Magaharibi ambapo amewataka wataalamu hao kufikisha ujumbe huo katika ngazi ya juu wa ajili ya utekelezaji.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema amekuwa akipokea malalamiko mengi ya wananchi kuhusu uuzwaji wa dawa za mifugo ambazo zimemaliza muda wake na hivyo kupelekea wananchi wengi kukosa imani na dawa hizo mwishowe kupoteza mifugo yao kutokana na magonjwa.

"Nimekutana na changamoto hii, wananchi wengi wanalalamika wanapewa dawa za kuosha ng'ombe ili kuuwa kupe lakini hawaoni magonjwa hayo yakimalizika na Wataalamu wetu wamefuatilia wamegundua dawa wanazouziwa wananchi hao ni feki na zingine zimekwisha muda wa matumizi".Mkuu wa wilaya.

Ni vizuri sasa wadau wetu wa mifugo kushirikiana na kuanza kufuatilia kwa karibu, kupita katika maduka hayo hata kwa kuanza na wale wasambazaji wakubwa ili tuweze kunusuru mifugo ya wafugaji inayokufa kila siku kutokana na kukosa dawa sahihi, ameongeza Mkuu huyo wa Wilaya.

Aidha DC Ludigija amewapongeza wananchi wanaoendelea kutembelea maonesho hayo na kuwataka kutumia elimu ya kilimo wanayoipata kupitia maonesho hayo kujiletea mafanikio lakini pia amewataka wananchu hao kuwapatia pia elimu hiyo wale ambao hawakuapata nafasi ya kutembelea maonesho hayo ili kuleta tija na mageuzi ya kilimo.

Mhe. Ludigija ametembelea maonesho hayo kujionea pia hali ya  maandalizi ya kilele cha nanenane ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda na kutoa maelekezo kadhaa kwa waandaaji wa maonesho hayo ili kuboresha sherehe za kilele hicho.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.