• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Elimu bure yazidi kuboreshwa Mwanza

Posted on: April 30th, 2018


Vitabu 47,930 vya kabidhiwa kwa halimashauri ya manispaa ya Ilemela ili kuboresha sekta ya elimu pamoja na kuondokana na changamoto ufundishaji na ujifunzaji.

Hayo yalibinishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  Mhe. John Mongella aliposema hauwezi kuzungumzia maendeleo bila ya elimu hasa ya msingi hivyo amekabidhi vitabu hivyo vya kusoma, kuandika, afya ya mazingira, michezo na sanaa, maarifa ya jamii na kingereza kwa ajili ya shule za msingi ili kuleta chachu ya usomaji kwa wanafunzi wa darasa la kwanza, pili na tatu.

Pia aliwataka wakuu wa shule kuhakikisha wanafunzi wanagawiwa vitabu na sio kuvifungia stoo ama kuviacha vikazagaa bali waazimishwe wanafunzi kwa utaratibu unaofaa na vitumike hata kwa vizazi vingine.

" Kila mtoto anatakiwa kuwa na kitabu kimoja wapewa hivyo vitabu hatutaki kukutana na watoto wasiojua kusoma hasa wa darasa la kwanza hadi la tatu na wakuu wa shule wenye tabia za zamani za kufungia vitabu stoo kila ukienda anatoa vilevile na kusema amenunua vipya waache wakibainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao "alisema Mongella .

Pia aliwataka kuacha tabia ya kuwarejesha nyumbani watoto kwa namna yoyote endapo akifanya hivyo aanze kuandika barua ya kuacha kazi kwanza ndipo achukue jukumu la kumrudisha mtoto nyumbani aidha kwa kukosa viatu, nguo ama sababu yoyote Kwani katika sera ya mtoto haki moja wapo ni kupata elimu.

Aliongeza kuwa lengo kuu ni kuondokana na watoto wasiojua kusoma, kuhesabu na kuandika hivyo kwa Mkoa wote wa Mwanza wamepokea vitabu 500,446, vyenye thamani ya sh. 1,251,115,000 hivyo ni jukumu lililopo ni kuvitumia .

Mongella alisema wakati umefika wa walimu, maofisa elimu kata na wadhibiti ubora wa shule kuzingatia ufatiliaji ubora wa utoaji elimu ufundishaji na usomaji wa watoto ili kuleta uelewa na matokeo mazuri.

" Hasa hawa maofisa elimu kata wamejijengea tabia ya kudhani wao wapo likizo mwaka mzima kazi yao ni kuzungukazunguka na kutoa macho tu na kutokuwa na maana ya ufanyaji kazi wao zaidi ya kuwa vyanzo vya watoto kufeli na upatikanaji wa ziro mashuleni" alisema Mongella.



Kwa upande wake, Ofisa elimu Mkoa Mwl. Michael Ligola alisema watahakikisha ndani ya wiki moja shule zote zitakuwa vimepata vitabu na kuwataka walimu wote waliokuwa wanalalamikia upungufu wa vitabu kuvitumia ipasavyo vitabu hivyo na kujituma katika utendaji kazi wao ili kuijenga vyema sekta ya elimu .

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.