• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Elimu ya uzazi wa mpango yatolewa Mwanza

Posted on: May 10th, 2021

Asilimia 48 ya wanawake wanaobeba ujauzito  mara kwa mara( wenye nzao nyingi) walipoteza maisha mwaka jana  wakati wa kujifungua mkoani Mwanza.

Aidha ,Wilaya ya Ukerewe mkoani humo mwaka jana iliongoza kwa wanawake kufuata uzazi wa mpango kwa asilimia 48 ikifuatiwa na Mwanza jiji asilimia 43, huku Ilemela ikishika nafasi ya tatu kwa asilimia 42.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Mwanza na Mratibu Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto mkoani Mwanza, Secilia Mrema alipozungumza na mwandishi wa habari hii ofisini  kwake.


Alisema kiwango kidogo cha matumizi ya uzazi wa mpango kimechangia vifo vya wazazi na watoto wachanga hasa wanawake wanaozaa mara kwa mara.

Akizungumzia masuala ya afya ya uzazi, Secilia alisema kiwango cha matumizi ya uzazi wa mpango kwa mwaka jana kilifikia asilimia 39 kutoka asilimia 18 mwaka 2015.

Secilia alisema kiwango cha uzazi wa mpango kimeongezeka huku vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga vikipungua mkoani humo.

Alisema mafunzo kwa watoa huduma za uzazi wa mpango zimeongezeka kutoka asilimia 35 mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 45 kwa mwaka jana.

Kwa upande mwingine,Secilia alisema bado kuna uelewa mdogo kwa wananchi kuhusu uzazi wa mpango pamoja na upungufu wa watumishi wenye ujuzi wa kutoa huduma za afya.

Aidha, alisema sekta hiyo bado inakabiliwa na upungufu wa vifaa vya kutoa huduma za uzazi wa mpango ikiwamo (IUCD kits)pamoja na kukabiliwa na uhaba wa watumishi wenye ujuzi wa kutoa njia za uzazi wa mpango baada ya kujifungua.

Kwa upande wake, Ofisa Mahusiano wa Kanda ya Ziwa wa shirika la Marie Stopes Tanzania, Shamim Abdallah alisema wanafanya kazi kwa ushirikiano na mkoani Mwanza, lengo likiwa ni kutoa elimu, kufundisha watoa huduma ili kuwafikia watu wengi husani wananchi wanaoishi visiwani.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.