• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HALMASHAURI YA ILEMELA YAPATA HATI SAFI MIAKA 5 MFULULIZO RC MTANDA AIPONGEZA

Posted on: June 26th, 2024

HALMASHAURI YA ILEMELA YAPATA HATI SAFI MIAKA 5 MFULULIZO RC MTANDA AIPONGEZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Halmashauri ya Ilemela kwa kupata hati inayoridhisha kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesbu za Serikali (CAG) kwa miaka mitano mfululizo.

“Halmashauri hii imepata hati inayoridhisha kwa miaka mitano mfululizo, mkipata hati hii maana yake ni kwamba hata msimamizi wa Halmashauri na Wilaya kwa ngazi ya Mkoa ni Mkuu wa Mkoa hivyo na Mimi nimepata hati inayoridhisha hongereni sana".  RC Mtanda katika kikao cha Baraza maalumu  la Madiwani kilichojadili taarifa ya CAG ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo mapema leo Juni 26, 2024.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa amelitaka Baraza la Madiwani kuendelea kusimamia menejimenti ya halmashauri hiyo ili kuhakikisha inaendelea kupata hati inayoridhisha au safi miaka ijayo.

Aidha, RC Mtanda ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuwa na hoja chache ambapo jumla walikuwa na hoja 29 za muda mrefu ambapo hoja 21 zilishafungwa na Halmashauri imebaki na hoja 8 za kujibu.

"Nimekuwa nikisikiliza hizi hoja nane na nimeridhika kuwa hoja hizi zitafutwa kwa kuwa mipango ya kuzifuta ipo na inawezekana, ninaiagiza Halmashauri hii kuhakikisha inajibu na kutekeleza kwa wakati hoja zote nane ambazo hazijatekelezwa".Mtanda

Mkuu huyo wa Mkoa ameitaka Halmashauri hiyo kuwasilisha mpango wa utekelezaji wa hoja zilizobaki kwa Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa na namna zitakavyotekelezwa na kuziondoa kabisa ifikapo tarehe 28 mwezi wa sita mwaka huu.

Mhe. Mtanda amesisitiza pia kuhusu ushirikiano baina ya Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Ilemela na Ofisi ya CAG kwa hesabu za mwaka 2023/2024 ili waweze kuondokana na Hoja.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Mhe. Renatus Murunga ameahidi kutoa ushirikiano na kufanya kazi kwa bidii ikiwemo kuyasimamia maagizo yote yaliyotolewa na Mhe. Mkuu wa Mkoa, aidha amesema yuko tayari kwenda na kasi ya Mkuu huyo wa Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.