• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID KUONGEZA UELEWA WA HAKI NA MASUALA YA KISHERIA - WAZIRI NDUMBARO

Posted on: February 18th, 2025

KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID KUONGEZA UELEWA WA HAKI NA MASUALA YA KISHERIA - WAZIRI NDUMBARO


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Damas Ndumbaro amesema uwepo wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia “Mama Samia Legal Aid Campaign” imesaidia kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu masuala ya haki, mifumo ya kisheria iliyopo, haki za binadamu na haki za makundi maalumu.

Mhe. Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo tarehe 18, Februari 2025 katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba na  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda wakati wa uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia katika katika viwanja vya Furahisha Wilayani Ilemela.

Aidha Mhe. Ndumbaro amesema kampeni hiyo imesaidia mifumo ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala na masuala ya upatikanaji haki kwa ujumla.


“Kwa kuzingatia utelezaji wa kampeni hii, niwaombe wananchi watumie fursa hii, ili kumaliza migogoro hususani ya madai kwa njia za usuluhishi”.

Waziri huyo amesema pia Viongozi wa ngazi ya juu wana imani kubwa kwamba kupitia kampeni hiyo na elimu itakayotolewa, watendaji pamoja na wananchi watapata uelewa wa masuala ya kisheria, migogoro mingi iliyokuwepo katika ngazi za kijamii itatatuliwa na wananchi watapata huduma za msaada wa kisheria kwa urahisi na ufanisi.

“Hakika kundi la wananchi wanyonge, wanaoishi pembezoni na wasio na uwezo litakuwa limefikiwa kwa kiasi kikubwa na wengi sasa hawatapoteza muda mwingi katika kushughulikia changamoto zao za kisheria bali watajikita katika shughuli za maendeleo”. Ameongeza Waziri Ndumbaro.

Kabla ya kuhitimisha hotuba hiyo Mhe. Mtanda ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kujitokeza kwa wingi kupata huduma za msaada wa

kisheria zinazotolewa kwani masuala ya kisheria ni masuala mtambuka ambayo mwananchi anapaswa kuyafahamu na si kusubiri hadi upate changamoto.

“Kwetu sisi wana Mwanza ni upendeleo wa kipekee, msipoteze kabisa fursa hii adhimu”.

Tangu Kampeni hii ilipozinduliwa tarehe 22 Aprili, 2023 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) imetekelezwa katika Mikoa Kumi na saba (17) ya Tanzania Bara na leo tarehe 18 Februari, 2025 kampeni hii inazinduliwa katika Mkoa wa Mwanza na tarehe 19 Februari, 2025 Kampeni hii itazinduliwa katika Mkoa wa Lindi. hali hii inafanya jumla ya mikoa 19 kufikiwa na kampeni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.