• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Workshop to complete the recruitment of new employees held in Mwanza

Posted on: September 28th, 2018


Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  kwa kushirikiana Taasisi ya Benjamini Mkapa na  Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa kupitia mradi wa Mfuko wa dunia wa kupambana na magonjwa ya Kifua kikuu,Malaria, na HIV/AIDS(GFATM)na mradi wa Mkapa Fellows Program awamu ya tatu,imeendesha kikao kazi cha kukamilisha mchakato wa ajira na kuwapangia vituo vya kazi wataalamu mbalimbali wa kada za afya ambao wanatakiwa kuripoti katika  vya kazi kuanzia Septemba 25, 2018.

Akiongea katika kikao hicho cha watumishi wa ajira mpya kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  Bwana  David M. Mnkhally  Afisa kutoka Taasisi ya Benjamini Mkapa amesema orodha ya majina ya watumishi wote waliopangiwa vituo vya kazi yanapatikana kupitia tovuti ya OR- TAMISEMI ambayo ni www.tamisemi.go.tz pia katika tovuti yaTaasisi ya Benjamini Mkapa ambayo ni www.mkapafoundation.or.tz.

Mradi huu wa RSSH unatekelezwa katika Mikoa kumi ya Tanzania bara, Mikoa hiyo inajumuisha Mwanza,Shinyanga,Mara,Simiyu,Geita,Kagera,Tabora,Katavi,Kigoma na Dodoma.Ambapo jumla ya watumishi 281 wataajiriwa katika Halmashauri mbalimbali katika Mikoa tajwa hapo juu,kwa Mkoa wa Mwanza jumla ni 23, kupitia mradi wa RSSH 19 na MFP III  ni 4.

Naye  Miyeye Yahya ambaye ni Afisa kutoka Taasisi ya Mkapa ameongeza kuwa ajira hizi ni za mkataba wa mwaka mmoja na zinasimamiwa na Taasisi ya Benjamini Mkapa hivyo basi watumishi wote waliopata fursa hii watapata kipaumbele cha kujiunga na utumishi wa Umma baada ya kukamilika kipindi cha mkataba,kulingana na upatikanaji wa ajira.


Aidha Bwana Deogratias Kayombo ambaye ni Afisa Utumishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia Wazee na Watoto (Afya) amesema kila mtumishi ahakikishe anazingatia misingi ya uwajibikaji na kukidhi maadili ya utumishi wa Umma katika utoaji wa huduma kwa Jamii.

Hata hivyo, Bi Hawa Waziri ambaye ni Afisa Utumishi Wizara ya Afya amesisitiza utii wa sheria katika Masuala kazi na nidhamu  ambapo amewataka watumishi kufanya kazi kwa weredi bila kubagua mtu yeyote katika kutimiza wajibu wao.

"Hakikisheni mnatimiza wajibu wenu na kuukamilisha kwa muda uliopangwa na kwa weredi,haitakiwi kutoa huduma kwa upendeleo fulani ikiwa ni pamoja na ushawishi wa kisiasa au kidini,"alisema Hawa.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.