• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maadhimisho ya Siku ya Unywaji wa Maziwa Shuleni kufanyika Mwanza

Posted on: September 23rd, 2023

Maadhimisho ya Siku ya Unywaji wa Maziwa Shuleni kufanyika Mwanza


Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewakaribisha wananchi wote wa Mkoa wa Mwanza na mikoa ya jirani kwenye maadhisho ya siku ya unywaji wa maziwa shuleni yatakayofanyika kwenye viwanja vya furahisha jumatano ya Septemba 27, 2023.

Mhe. Makilagi ametoa wito huo leo tarehe 23 Septemba 2023 wakati wa mkutano wa Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla na waandishi wa habari ambapo alizungumza kwa niaba yake kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Makilagi amesema unywaji wa maziwa shuleni unachangia kuwapa afya njema watoto, kuboresha ukuaji wa mtoto, kupata matokea mazuri kwenye taaluma, kuanza mapema tabia ya umuhimu wa matumizi bora ya lishe, kuhudhuria masomo bila kukatisha na kuondoa utoro.

"Maziwa yanasidia kumfanya mtoto kuwa na afya bora na hali hii inachangia sana hamasa ya kujifunza na kuwafanya watoto kupenda shule tofauti kabisa na watoto wasiopata maziwa shuleni na watoto wakijengwa hivyo inasaidia kupanua ufaulu." Amesema Mhe. Mkuu wa Wilaya.

Vilevile, amefafanua kuwa kilele cha maadhimisho hayo kitatanguliwa na shughuli mbalimbali kama ugawaji wa maziwa kwenye shule kumi za watoto wenye mahitaji maalum zaidi ya 450 siku ya tarehe 25, Septemba 2023 na siku ya jumanne kutakua na kongamano la wadau kuhusiana na maadhimisho hayo katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa.

"Hali ya unywaji wa maziwa kwa sasa nchini bado iko chini kwani kwa mwaka inatakiwa mtu anywe lita 200 lakini mtanzania kwa sasa anakunywa lita 62  tu na lengo la maadhimisho haya ni kutoa elimu ya umuhimu na kuhamasisha watu kunywa maziwa." Amesema Deogratias Buzuka, Afisa uzalishaji Maziwa Bodi ya Maziwa Tanzania.

Katika kuchagiza matumizi bora ya maziwa kwa ukuaji na kujenga siha njema kwa jamii, maadhimisho ya siku ya unywaji wa maziwa nchini mwaka 2023 yanaenda na Kaulimbiu isemayo 'Mpe Mtoto Maziwa kwa maendeleo bora shueni'.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.