• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mafundi simu waonywa kununua simu za wizi

Posted on: April 7th, 2019


Jeshi  la Polisi Mkoa wa Mwanza  limesema tayari limenasa mtandao wa mafundi simu ambao wananunua simu za wizi  zenye thamani kubwa na kwenda kuziuza au kubadilishana na wahalifu wa  nchi jirani na Kenya ambao hukutana mpakani.

Akijibu maswali ya wadau  mbalimbali katika simina iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa watoa huduma za mawasiliano nchini, Mussa Zuberi kutoka kitengo cha makosa ya mitandao Mkoa wa Mwanza, alisema mtandao huo umebainika baada ya kuanza kuwakamata mafundi simu na kuwahoji.

 Alisema kwamba baada ya jeshi la polisi kupokea kesi nyingi za upotevu wa simu na kufuatilia ilibainika hupelekwa kwa mafundi simu ambao huziondoa namba ya siri na kubadilisha namba ya utambulisho  yaani IMEI kwa matumizi.

TCRA imeandaa simina kwa wadau mbalimbali  wakiwamo kampuni za mawasiliano Tanzania, viongozi wa umoja wa mafundi simu, waandishi wa habari, viongozi wa dini  na wadau wengine wa sekta hiyo ikiwa  lengo ni kukumbushana taswira ya sheria ya makosaya mitandao ya mwaka 2015 na changamoto zinazojitokeza.


Zuberi alifafanua kwamba  baadhi ya simu zingine ambazo mafundi hao huzinunua huzipeleka mpakani mwaka Kenya na Tanzania na kuziuza au kubadilishana na mafundi wa Kenya jambo ambalo huwafanya polisi kitengo cha  mkoasa  ya mitandao kupata ugumu wa kuzipata kwani huwa hazionekanani katika mfumo wa mtandao.

“Mpaka tunapozungumza  sasa tayari baadhi ya mafundi   wanashikiliwa kwa vitendo hivyo na wametueleza namna biashara hivyo inavyofanyika, wanakwenda kule mpakani Sirari upande wa Tanzania wanakutana na wenzao wa Kenya wanabadilishana au kuuziana hizo simu za wizi, ndio maana mtu anaweza kuleta malalamiko tukashindwa kuipata simu yake.

“Tunapoitafuta kwenya mfumo wa mtandao wetu haipatikani kwani inakuwa nje ya Tanzania lakini mtumiaji yule anapokuja upande huu huwa inasomeka kwa muda na kutoweka sasa inakuwa  vigumu  kuifuatilia kwani tunakuwa mbali na mhalifu.

“Kikubwa tunachowaomba mafundi simu watambua kitendo cha kuanza kuchokonoa simu kwa kufuta namba ya siri iliyowekwa na mhusika sambamba na IMEI ni kosa, kosa la pili ni kuuza mali za wizi, hivyo tumewataka kuacha biashara hiyo na kushirikiana na polisi kuwakamata wale wanaowapelekea simu,”alisema.

Zuberi alisema hivi sasa wanatarajia kukutana na watu wa idara ya uhamiaji kuona namna kufanya ukagazi mpakani Sirari mkoani Mara  katika  mabegi ya abiria na pale wanakuta mtu akiwa na simu nyingi ambazo hazimo katiba maboksi rasmi au kutokuwa na stakabadhi za manunuzi zinapaswa kushikiliwa kwa mahojiano zaidi.

Hata hivyo alisema baadhi ya watu walioibiwa simu zao hukata tamaa pale anapotakiwa kutoa ushirikiano  ambapo alitoa wito kwa jamii kuwa waangalizi katika matumizi ya simu zao za mikononi kwa kuepuka matusi na kusajili laini ambayo taarifa zake si kweli.

Naye Mkuu Msaidizi wa Kitengo cha uhalifu wa kimtandao kutoka makao makuu ya jeshi la polisi, Joshua Mwangasa alisema tangu mwaka 2015 takwimu za makosa yamekuwa yakiongezeka na kupungua.

“Ukiangalia mwaka 2015 tulipokea makosa 5,172,  2016  (9,441),  2017 (7889) na mwaka 2018 tulipokea 8,708  hapo utaangalia yanapanda na kushuka lakini nasema tunakoelekea 2020 tunakwenda katika kiwango cha juu cha matumizi ya teknolojia ambacho kila mtu shughuli zake zitakuwa kwenye simu.

“Tukumbuke hata vitabu vitakatifu vimeandika siku za mwisho maarifa yataongezeka hivyo kuanzia mwaka 2020 watanzania wataanza kutumia kiwango cha 5GB, ni lazima sasa kama polisi na TCRA tukaanza kutoa elimu ya kuwalimisha namna ya kuepuka kuingia kwenye makosa ya jinai.

“Matokeo ya matumizi mabaya ya mtandao wa kijamii yamegawanyika sehemu tatu, kwa upande wa kijamiini  unaleta mmomonyoko wa maadili, upande wa siasa inaleta uvunjifu wa amani na kundi la mwisho ni lipo kwenye uchumi na athari zake ni kuharibu mfumo muhimu wa kitaifa,”alisema.









Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.