• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAGEUZI YA SERA YA ELIMU YATACHANGIA WINGI WA UJUZI NA VIJANA KUJIAJIRI-WAZIRI MKENDA

Posted on: July 5th, 2023

MAGEUZI YA SERA YA ELIMU YATACHANGIA WINGI WA UJUZI NA VIJANA KUJIAJIRI-WAZIRI MKENDA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof.Adolph Mkenda amesema mageuzi yajayo ya Sera ya Elimu nchini yatakayojikita kumuongezea ujuzi zaidi kijana akiwa shuleni yatachangia vijana wengi kujiajiri kulingana na mazingira yanayomzunguka.

Waziri Mkenda amesema hayo Julai 05,2023 wakati wa majumuisho ya ziara yake ya siku moja Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza baada ya kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara yake vikiwemo vyuo vya ufundi Veta,amebainisha mafunzo ya Amali kama yanavyojulikana yataanza muda siyo mrefu mara baada ya Sera hiyo kupita kwenye hatua za mwisho mwisho.

"Sera hiyo mpya itamtaka mwanafunzi kuwa shuleni kwa miaka kumi tu atasoma hadi darasa la sita akifaulu atalazimika kuingia kidato cha kwanza hadi cha nne huko sasa atakutana na mafunzo kwa vitendo zaidi na akihitimu anatoka na ujuzi husika utakaokuwa mkombozi katika shughuli aliyolenga", amefafanua Prof Mkenda.

Kiongozi huyo mwandamizi wa Serikali ameongeza kuwa Mkoa kama wa Mwanza mafunzo hayo ya Amali yatawanuisha wale watakaojikita kwenye Uvuvi kwani wakihitimu watakuwa na ujuzi wa kutosha kwenye sekta hiyo tofauti na ilivyo sasa.

Waziri Mkenda amebainisha utekelezaji huo ni ahadi ya Rais Dkt.Samia Suluhu aliyoitoa Bungeni ya kuleta mageuzi kwenye sekta ya elimu kwa kutaka yawepo mafunzo zaidi ya kuwaongezea ujuzi ili kuweza kuzimudu fursa mbalimbali zilizowazunguka.

"Huu mchakato wa sera mpya ya elimu umeanza siku nyingi kwa kuwashirikisha wataalam na wadau,nawathibitshia sasa upo ukingoni kusubiri hatua kadhaa za mwisho mwisho za kupitiwa na Makatibu wakuu na Baraza la Mawaziri kabla ya kumfikishia rasmi Rais ili kumuomba aridhie,"Prof.Mkenda

Akiwa kijiji cha Karumo Wilayani Sengerema Waziri Mkenda ameshuhudia maandalizi ya ujenzi wa Chuo Kikuu Ardhi Kampasi ya Mwanza kitakacho kamilika Octoba mwakani kilichoghalimu zaidi ya Shs bilioni 18.

"Mhe Waziri Chuo hiki kitachukua muda wa miezi 15 kukamilika na kuanza kutoa mafunzo,wiki chache zijazo tunatarajia kumpata Mkandarasi,hapa kutakuwa na kozi 35 zikiwemo za kuwapata Wataalamu wa kupima ardhi kupitia majini, watatuzi wa migogoro ya ardhi na mafunzo ya amali pia yatatolewa hapa chuoni,"Prof.Evaristo Liwa,Makamu Mkuu Chuo Kikuu Ardhi.

Aidha Waziri Mkenda ameshauri mara baada ya Chuo hicho kukamilika kuwepo na mpango wa kuwapata baadhi ya wahadhili kutoka nje ya nchi watakaongeza utoaji wa elimu bora na kubadilishana uzoefu na watalaam wa hapa nyumbani.

Waziri huyo wa Elimu,Sayansi na Teknolojia akiambatana na Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Seni Ngaga amefika Halmashauri ya Buchosa na kushuhudia maandalizi ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Veta kitakachoghalimu Shs bilioni 3.


Pia akiwa mjini Sengerema amekubali kukipokea Chuo cha Ufundi Veta mara baada ya uongozi kuwasilisha barua rasmi ya ombi hilo,  awali Chuo hicho kilikuwa kinamilikiwa na Halmashauri ya Sengerema.

"Mhe Waziri tumefarijika na ujio wako ambao kwa kweli umetutia shime na mpango ujao wa sera mpya ya elimu,tumejipanga vizuri kuongeza maeneo kwa ajili ya kuongeza madarasa yatakayo kidhi mpango huo wa Serikali ambao utakuwa ni muorobaini wa ukosefu

 wa ajira kwa vijana wetu,"Seni Ngaga,Mkuu wa Wilaya Sengerema.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.